HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 24, 2024

SEKTA YA UWEKEZAJI YAPANDA KWA ONGEZEKO LA 8.6%

THAMANI ya  uwekezaji  katika Taasisi  zinazo simamiwa  na ofisi ya Msajili na Hazina  yameongezeka  kutoka Shilingi Trilioni 70 katika kipindi cha mwaka 2021 hadi  kufikia  Shilingi Trilioni 76 mwaka 2023 sawa na ongezeko  la 8.6%.



Yamesemwa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Mobhare Matinyi Machi 24 2023 alipozungumza  na wahariri na waandishi  wa habari  katika mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam. 

Matinyi amesema kuwa  Ofisi ya Msajili wa Hazina imeongeza  makusanyo  ya mapato yasiyo ya kodi  kutoka Bilioni 637.66 hadi Trilioni 1.008 kwa mwaka 2023 sawa na  ongezeko  la 58%.



"Serikali  imeongeza  umiliki  wa hisa katika Kampuni  ya Almasi ya Williamso  Diamonds kutoka  25%hadi 37%huku ikisaini mikataba  ya ubia  wa 16% zisizohamishika katika Kampuni  za madini"amesema Matinyi.

 

"Katika  kipindi  cha kuanzia Machi 2024 hadi Februari  2024  Wizara  ya Madini  imefanikiwa  kujiendeleza  sekta  kwa namna mbalimbali  ikiwemo  kukusanya  maduhuli  na kufikisha  kiasi cha  Shilingi Trilioni 1.93 awali  mwaka 2021/22 ilikuwa Shilingi. Bilioni 591.5 lakini  hadi kufikia 2023/24 imefikia Shilingi Bilioni 690.4.



Aidha Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi, amesema kuwa  Tanzania imeendelea kuwa katika kundi la nchi zenye uchumi wa pato la kati ikimaanisha pato la wastani la kila mwanachi kwa mwaka (GNI per capital) ambapo ingawa mwaka 2019 ilikuwa kiasi cha dola 1,080 (Tsh. 2,743,813) lakini mwaka 2022 ni dola 1,200 ( Tsh. 3,048,681).

 

“Uchumi wa Tanzania umeendelea kukua licha ya athari kubwa za mripuko wa UVIKO-19 duniani pamoja na vita za Urusi na Ukraine na pia katika nchi za  Mashariki ya Kati matatizo haya yaliutikisa uchumi wa dunia na  Tanzania ambao ulikuwa umefikia wastani wa ukuaji wa zaidi ya 7% na kuushusha hadi 4.2% mwaka 2020" amesema.



“Hata hivyo, hivi sasa ukuaji umefikia 5.2% kutokana na uongozi thabiti wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais  Dkt.Samia Sukuhu Hassan, aidha Tanzania imeendelea kuwa katika kundi la nchi zenye uchumi wa pato la kati, ikimaanisha pato la wastani la kila mwanachi kwa mwaka (GNI per capital) ambapo ingawa mwaka 2019 ilikuwa kiasi cha dola 1,080 (Tsh. 2,743,813) lakini mwaka 2022 ni dola 1,200 ( Tsh. 3,048,681)".



“Serikali  imeendelea kudhibiti mfumuko wa bei ambapo kwa sasa ni chini ya 4% - kiwango ambacho ni miongoni mwa viwango bora katika nchi za jumuiya za kikanda ambazo Tanzania ni mwanachama, kama Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)”amesema Matinyi. 



“Akiba ya fedha za kigeni imeendelea kuwa toshelezi ambapo katika kipindi chote cha miaka mitatu hadi Desemba 2023, nchi ilikuwa na akiba inayotosha kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi kwa miezi 4.5, ikiwa ni kiwango cha juu ya lengo la miezi 4, akiba hiyo ni sawa na dola za Marekani bilioni 5.4”




No comments:

Post a Comment

Pages