HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 17, 2024

BITEKO AZIASA BENKI KUENDELEA KUDHAMINI MANESHO YA WAFUGAJI KIBIASHARA

 

Naibu Waziri Mkuu Dk. Doto Biteko (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Kilimo, Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Christopher Mwalugenge (wapili kushoto) alipotembelea Banda la benki ya NMB katika sherehe za ufungaji wa maonesho na mnada wa mifugo uliyofanyika katika Kata ya Ubena Zomozi wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Ushauri Kilimo wa Benki ya NMB, Isaac Masusu na wapili kulia na meneja Mwandamizi idara ya Bima wa Benki ya NMB, Catherine Joshua (Na Mpiga Picha Wetu).

 

Na Mwandishi Wetu

 

NAIBU Waziri Mkuu   Dotto  Biteko ametoa wito kwa Wadau wezeshi wa wafugaji nchini kuendelea kutoa elimu na mikopo ili waweze kufuga kibiashara wapate tija katika ufugaji wao.

Amewataka wadau wezeshi hao kutoishia kwa wafugaji wa kibiashara  bali wawafikie  wafugaji wa kienyeji ili na wao waweze kuwa wafugaji wenye tija nchini  kwani hilo ndilo lengo la serikali ya awamu ya sita ambayo inalenga kuwanyanyua wafugaji.


Naibu Waziri Mkuu Biteko amesema hayo leo  Juni 16  wakati akifunga maonesho hayo ya siku tatu  ambayo yamefanyika Ubena Zomozi  ,Halmashauru ya Chalinze  Mkoani Pwani.

Naibu Waziri Mkuu amefunga monesho hayo akimwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye amepata udhuru , hivyo natoa  wito huu kwa uongozi  wa Benki zulizo toa  udhamini huu ambazo ni Benki ya Kibiashsra ya Kilimo TADB na NMB  kundelea  kutoa elimu  kwa wafugaji kwani wao wamekuwa wakichangia migogoro na wakulima kutokana na kwenda kulisha mifugo yao kwenye  mashamba.

"Halmashauri za wilaya nchini  zitunze maeneo ambayo yalitengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo"

Serikali itaendelea kuunga mkono maonesho  ya Wafugaji wa Kibiashara nchini ili waendeleze haya maonesho ambayo yanatoa elimu na kutoa Uhalisia wa ufugaji wa kibiashara utakaoongeza tija kwa wafugaji na kupata soko katika soko la kimataifa.

"Maonyesho haya muyapeleke katika ngazi za Kanda ambako yatakutana walengwa ambao ni wafugaji wa kienyeji  na wawape elimu wabadilike na kufuga kibiashara".

"Wafugaji wanapitia changamoto nyingi  hivyo hivyo msichoke kuwapa elimu ya ufugaji  wa Kibiashara nina imani watabadilika taratibu na badaye nchi itakuwa na wafugaji wenye mifugo yenye faida.

"Msiwasahau wafugaji wanaofuga kienyeji  na mwakani naomba  baadhi wawepo kwenye maonesho haya kwani watakapokuja watajifunza  na kubadilika"amesema Biteko.

Wakati huohuo  amewaonya wafugaji  kuacha migogoro  na wakulima  na kuacha tabia ya  kupitisha mifugo  yao kwenye mashamba ya wakulima  huku akiwasisitiza elimu itumike pamoja na sheria katika kumaliza migogoro hiyo.

"Hivi sasa dunia  inakwenda kidigitali hivyo hatakwa sisi ambao tulilelewa katika familia za wafugaji nawaasa mbadilike msiwe kama  wafugaji wa zamani ambao walikuwa wakifuga na kulalia ngozi lakini wafugaji wa kisasa wanalalia magodoro hivyo nanyi mbadilike sasa mfuge mifugo itakayowaletea tija acheni kufuga kizamani" amesema Biteko.

Akiwa katika banda la Benki ya Maendeleo ya kilimo nchini TADB akizungumza  kwa niaba ya Mkurugenzi Mwendeshaji wa TADB David Nghambi amesema kuwa  Benki  hiyo kipindi cha miaka mitatu wametoa mikopo ya zaidi ya  Bil.13, wamewawezesha wafugaji kibiashara ili wawe na uhakika wa masoko kimataifa kwa kunenepa mifugo, pia wametoa mikopo ya bilioni 47 kwa wafanyabishara wa maziwa.

Aidha akikagua banda la NMB Mheshimiwa Biteko amezindua huduma ya Bima kwa mifugo ambayo ni 20,000 kwa mwana na  inatoa kinga dhidi ya vifo vya mifugo vitanyotokana na radi,  majeraha ya ndani na nje kwenye eneo la usafiri, moto, dhoruba, kung'atwa na nyoka mafuriko, magonjwa ya asili na yasiyodhibitika kwa mifugo.

No comments:

Post a Comment

Pages