HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 04, 2024

CHAMA AAGA KIUME UNYAMANI

Na Mwandishi Wetu

 

Matanga yameanuliwa kila mmoja na kwake, ila nyakati zitakumbukwa kwa washirika wa juzi na jana ndivyo unaweza kuelezea katika kile kinachoendelea kwa Wekundu wa Msimbazi Simba baada ya kuachana na Mwamba wao Clatous Chota Chama.


 

Baada ya Clatous Chota Chama kumaliza mkataba wake wa kuichezea Simba SC June 30, 2024 na kisha July 01,2024 akatambulishwa rasmi kama Mchezaji mpya wa Yanga SC, leo July 03,2024 Chama amewaaga rasmi Simba na kuwashukuru kwa kumfanya kuwa bora zaidi.

 

Chama anaondoka Simba SC baada ya kuitumikia kwa miaka 6 katika vipindi viwili tofauti ambapo alijiunga Simba SC kwa mara ya kwanza 2018 akitokea Lusaka Dynamos ya Zambia na kisha 2021 kuondoka Simba SC na kujiunga na RS Berkane aliyodumu kwa msimu mmoja na kurejea Simba SC 2022.

 

Kwenye taarifa aliyoitoa leo Chama amesema miaka sita iliyopita alifika Simba kama Mgeni na Club hiyo ikamfanya kuwa bora zaidi ya alivyokuwa kabla na akawa sehemu ya Watu walioitawala ardhi na kuifanya Simba kupanua zaidi himaya yake hadi sehemu nyingine za Afrika.

 

Chama amesema baada ya miaka sita ya furaha, fahari na kusudi ameamua kuondoka Simba huku akitoa heshima kwa kila mmoja ndani ya Simba kwa upendo na ushirikiamo aliopewa kwa miaka yote “Hakuna Mtu anayeweza kubadilisha historia tuliyotengeneza pamoja”

 

“Wanasema shoo haijaisha mpaka Mwanamke mnene aimbe na ninaamini huu wimbo utawapatia thamani ya muda wenu, nawatakia kila la kheri, tutaendelea kuonana, nguvu moja”



No comments:

Post a Comment

Pages