HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 01, 2024

Rais Dkt. Samia ampokea rasmi Msigwa wa CHADEMA

 

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akipeana mkono na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ambaye amejiondoa kutoka chama hicho na kujiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Juni 30, 2024, jijini Dar Es Salaam.

Msigwa amesema amechukua uamuzi huo baada ya kuona Chadema kimepoteza uhalali wa kuwa mkosoaji wa CCM, lakini pia kuunga mkono juhudi za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayofanya ya kuiongoza nchi na kuwatumikia Watanzania. Pia baada ya kuchoshwa na siasa za uongo, unafiki na kiulaghai zinazofanywa na Chadema.






No comments:

Post a Comment

Pages