Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Jeshi
la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia Watu 10 kwa
tuhuma ya kuenndesha Televisheni Mitandao bila ya kuwa na leseni.
Akizungumza
na wanahabari leo jijini humo Kamanda wa Kanda hiyo Jumanne Muliro
amesema kuwa kati ya Oktoba 3 hadi 10 mwaka huu walfanikiwa kuwakamata
watu wakiendesha televisheni hizo bila ya kuwa leseni za mamlaka husika
huku akisisitiza ni kinyme na sheria ya uendeshaji wake.
"
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata
watu 10 wakiendesha televisheni mtandao bila ya leseni hii ni kinyume na
sheria," amesema Kamanda Muliro.
Amewataja
miongoni mwa watuhumiwa hao ni Japhet Lekingu, Joseph Augustino wote wa
Wakazi wa Ukonga Sabasaba, Tegemea Mwinyigoha ( mkazi wa Tabata na Elias
Pius makzi wa Mbezi Juu.
Amesisitiza kuwa
watuhumiwa wamekutwa wakiendesha televisheni hizo bila ya kufuata sheria
na kanuni za uendeshaji wake na kwamba watafikishwa mahakamani kwani
upelelezi umekamilika.
Katika hatua nyingine,
Kamanda Muliro Jiji la Dar es Salaam liko katika hali ya usalama huku
akibainisha wananchi wanaendelea na shughuli zao kwa amani na utulivu.
Amefafanua
kuwa wananchi wanashiriki kampeni za Wagombea wa Uchaguzi Mkuu kwa
kusikiliza sera zao hivyo amewasisitiza wananchi kwenda kupiga kura
Oktoba 29, 2025 ni haki yao ya Kikatiba.



No comments:
Post a Comment