HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 20, 2025

MBETO: DKT. MWINYI YUPO TAYARI KUWATUMIKIA WANANCHI

Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema Mgombea wake wa nafasi ya Rais Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi  yuko imara, akijiandaa kutwaa ushindi  wa kidemokrasia ili kuiongoza tena Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar  (SMZ), kipindi cha pili.


Dkt. Mwinyi ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kufikia  hatua hiyo anajivunia mafanikio aliyopata katika kutimiza kwa vitendo ahadi zake kwa wananchi na Ilani ya chama chake.


CCM, kimesema Makamu Mwenyekiti  wa ACT  Wazalenzo, Ismail Jussa  Ladhu na chama chake hawana cha kuwaeleza wananchi kwani yote yametekelezxwa na Dkt. Mwinyi na kupitiliza.



" Jussa atabaki kuwa legelege na tepetepe kwakuwa  hayo ndio maisha alioyachagua kuishi na wenzake" alisema Katibu wa Kamati Maalum ya NEC  Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis, ameeleza hayo akijibu madai ya Jussa aliyedai kuwa Rais Dkt. Mwinyi yuko tepetepe kwa akihofia  kushindwa Uchaguzi.


Mbeto  alisema kwa haiba na  ustawi wa mabadiliko ya  maendeleo makubwa yaliochomoza  chini ya uongozi wa Rais  Dkt. Mwinyi ni ujinga na upuuzi mtu kusema  kiongozi  huyo atashindwa uchaguzi .


Alisema  siku zote wananchi wanahitaji kuona serikali yao ikiwatumikia kwa kuwaletea  maendeleo ikiwemo kuimarika kwa huduma za kijamii na wananchi wakifaidika nazo .


Alisema Rais Dkt. Mwinyi yuko imara na madhubuti huku  akisubiri siku ya kutangazwa na kuwa Rais kwa kipindi  cha pili. 


'Kwakuwa tumejiandaa kushinda lazima tuibuke na ushindi usio na longolongo. Sera za chama chetu zimejibu changamoto zote zilizokuwa zikiwatatiza wanchi katika sekta za Maendeleo. Tumetimiza ahadi na wajibu wetu. Ni  haki yetu kupata ushindi wa kishindo" alisema Mbeto.


Katibu  Mwenezi  huyo aliongeza kusema mkataba wa miaka mitano iliopita kati ya wananchi na CCM ni utekelezaji wa   Ilani ya Uchaguzi. Kazi hiyo kimsingi imefanyika kwa weledi na umakini mkubwa na kukamilika" alieleza


"Rais ametekeleza ahadi za kisera na zile zake binafsi  hivyo hawezi  kushindwa na mgombea anayetaka achaguliwe ili akafanye majaribio ya kuongoza nchi. Serikali si  chumba cha maabara cha kufanyia majaribio" alisisitiza Mbeto.


Katibu huyo Mwenezi, amewahakikishiawananchi, wanachama wa CCM, wafuasi na Wakereketwa wake ,kujiandaa na kwenda kupig kura Oktoba  29 kisha wawe tayari  kupokea matokeo ya ushindi.  


"Jussa na wenzako  jiandaeni kushuhudia kimbunga  cha ushindi  wa CCM kikiwapeperusha .na hila na njama zenu zimekwama hivyo jipangeni kutoka machozi bila kilio "alijinasibu Mwenezi  huyo.

No comments:

Post a Comment

Pages