HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 23, 2014

TASO KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA

Ofisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group, Imani Kajula akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu ushirikiano wa kampuni hiyo na Umoja wa Wakulima Tanzania (TASO), katika kuhamasisha kilimo na maonyesho ya Nanenae yatakayoanza Agostii 1-8. Kulia ni  Mkuu wa Biashara EAG Group, Mathew Gugai na Mwenyekiti wa Taifa Taso, Engelbert Moyo. (Picha na Francis Dande)
 Mwenyekiti wa Taifa Taso, Engelbert Moyo akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.


Na Ramadhani Tembo 

KATIKA kuelekea sherehe za sikukuu ya wakulima na maonesho ya Nanenane yanayotarajiwa kufanyika Kitaifa katika Mkoa wa Lindi kuanzia Agosti 1-8, Jumuiya ya Wakulima Tanzania (TASO), wamejipanga kutoa mafunzo ya kilimo,uvuvi na ufugaji bora.

Maonesho hayo yanatarajiwa kufunguliwa na Rais wa Zanzibar Ally Mohamed Shein na kufungwa na Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa (TASO), Englibert Moyo,alisema katika sherehe hizo wakulima,wafugaji na wavuvi  watapata fursa ya kubadilishana uzoefu katika shughuli zao.

Alisema sherehe hizo zitahamasisha jamii  kuthamini kilimo kama mkombozi wa Watanzania na tunapaswa tujifunze njia mbalimbali za kilimo kufikia viwango vya Kimataifa.

Aidha kwa upande wa wafanyabiashara Maonesho hayo yatatoa fursa nzuri ya kutangaza na kupanua soko la bidhaa zao hususani pembejeo na zana mbalimbali za kilimo, uvuvi na ufugaji nyuki.

Pia aliwaasa wakazi wa Lindi na Mikoa ya jirani kuhudhuria katika Maonesho hayo yanayofanyika kwa mara ya kwanza mkoani humo.

No comments:

Post a Comment

Pages