HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 15, 2018

TULIA CUP 2018 YAZINDULIWA RASMI JIJINI MBEYA

NA KENNETH NGELESI,MBEYA
LIGI ya soka na Netiboli Tulia Cup 2018 imezinduliwa rasmi juzi katika Viwanja vya shule ya Msingi Ruanda Nzovwe jiji Mbeya huku mdhamini wa michuano hiyo Naibu Spika Dk Tulia Ackson akizitaka timu za ligi kuu zikiwemo Tanzania Prisons na Mbeya City FC kutumia michuano hiyo kusaka vipaji vya wachezaji watakao weza kuwatumia katika michezo mbalimbali ikiwemo ligi kuu.
Akizungumza mara baada ya ufunguzi wa Michuano Dk.Tulia alisema kuwa ligi hiyo itaanzia ngazi ya mitaa na baadaye kata 36 za jiji la Mbeya ,ngazi ya sita bora nusu fainali na hatimaye fainali zinazotarajiwa kupigwa Semptemba mwa huu.
Dk Tulia alisema ni fursa kwa timu za ligi kuu,daraja la kwanza na pili lakini pia ni fursa kwa wachezaji kuonyesha uwezo wao wa kucheza soka ili waweze kuonwa na timu kubwa .
‘Ni fursa kwa timu kusaka wachezaji lakini pia ni fursa kwa kwa vijna kuonyesha uwezo wao kwani mpira kwa sasa ni ajira na si soka tu lakini pia hata netibali itaenda sambamba kuanzi ngazi za mitaa na hatiamiye kata’
Michuano hiyo ilizinduliwa kwa kuzikutanisha timu ya Ilemi FC na Mbeya Youth mchezo uliomalizika Ilemi kuibuka na ushindi wa bao 1-0 Dk Tulia alisema michujo utaanzai ngazi mitaa kwa ajili ya kuoputa bingwa wa kata ambapo Tasisi yake “Tulia Trust” itatoa jezi pamoja na mpira kwa ajili ya michezo ligi hiyo timu zote za
Katika hatua nyingine Dk. Tulia alibainisha zawadi kuwa Bingwa katika michezo yote kila timu ataondoka na Bodaboda boda moja,Kombe,Medali kila mchezaji,Seti ya Jezi,na mpira,washindi wa pili medali kwa kila mchezaji,fedha taslimu sh.milioni 1.5,kombe,seti ya Jezi na Mpira.
Mshindi wa tatu ataondoka na fedha tasilimu milioni moja,seti ya Jezi,mpira na medali kwa kila mchezaji,huku mshindi wan ne akiondoka na shilingi lakini saba,700,000/ na watano shilingi laki tano na medali pia.
Pia Naibu Spika Dk Tulia alitangaza rasmi kugharamia masomo ya ziada Binti Diana Lucas wa kidato cha nne kutoka shule ya Sekondari Nzondahaki ya jiji Mbeya baada ya kufanya vizuri nafasi yan Ushambuliaji katika mchezo wa soka wasichina kwenye Mashindano ya UMISETA 2018 yaliyiomalizika hivi karibuni jiji Mwanza.
Kwa upande wake Mdau wa mchezo wa soka jiji Mbeya James Mwampondele alipongeza uamuzi uliofanywa na Naibu Spika huku akiahidi kutoa seti moja ya Jezi kwa timu zitakazo shika nafasi ya kwanza hadi ya nne.
“Mimi naunga mkono kazi hii ya Naibu Spika hivyo nikiwa kama mdau wa michezo nitatoa jezi seti moja kwa kila timu kuanzia ile ya kwanza hadi itakayo shika nafsi ya nne”

No comments:

Post a Comment

Pages