HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 20, 2019

WAMILIKI VIWANDA VYA KUCHAKATA MAGOGO WARUHUSIWA KUTUMIA MASHINE ZA ZAMANI

Meneja wa Shamba la Miti la North Kilimanjaro (Rongai)  Ernest Madata (Katikati) akimuongoza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu (kushoto)  alipotembelea vitalu vya miti katika shmaba hilo .kulia ni Afisa Misitu Emanuel Kiyengi.
Meneja wa Shamba la Miti la North Kilimanjaro (Rongai)  Ernest Madata akiumuonesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu sehemu ambayo huoteshwa mbegu za miti mbalimbali.
Meneja wa Shamba la Miti la North Kilimanjaro (Rongai)  Ernest Madata akimuonesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu sehemu ya vitalu vya miti vinavyoandaliwa na shamba hilo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu akitizama kitalu cha miti iliyo tayari kupelekwa shamba kwa ajili ya kuoteshwa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu akitizama mche wa mti uliooteshwa katika kitalu cha Shamba la Miti la North Kilimanjaro.
Sehemu ya vitalu vya miti katika shamba la miti la North Kilimanjaro .
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu akiotesha mche wa mti katika eneo la vitalu vya kuandaa miche ya miti katika shamba la miti la North Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu akimwagia maji mche wa mti aliuotesha katika eneo la vitalu vya kuandaa miche ya miti katika shamba la miti la North Kilimanjaro.
Meneja wa Shamba la Miti la North Kilimanjaro (Rongai)  Ernest Madata akumueleza jambo Naibu Waziri ,Kanyasu alipofika eneo ambalo shughuli ya uvunaji wa miti inafanyika.
Sehemu ya Msitu uliopo kwenye shamba la miti la North Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu akizungumza na watumishi wa Mashamba ya Miti ya North Kilimanjaro na West Kilimanjaro alipofanya ziara ya siku moja ya kutembelea mashamba hayo.
Baadhi ya watumishi wa Mashamba ya West Kilimanjaro na North Kilimanjaro wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Constantine Kanyasu .
Meneja wa Shamba la Miti la North Kilimanjaro ,Ernest Madata akizungumza katka kikao hicho.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii, Kanda ya Kaskazini


SERIKALI imeruhusu Wamiliki wa viwanda vya kuchakata Magogo kwa ajili ya kutengeneza Mbao kuendelea kutumia Mashine za zamani wakati wakiwa katika mchakato wa kujielekeza kwenye mabadiliko ya teknolojia .

Hatua ya serikali inatokana na ombi la Wadau wa misitu walilotoa wakati wa ziara ya siku Moja ya Naibu Waziri wa Malisili na Utalii ,Constantine Kanyasu alipotembelea Mashamba ya Miti ya North Kilimanjaro maarufu kama Rongai na West Kilimanjaro.

Mh Kanyasu pia akazungumzia suala la mgao mdogo wa Magogo kwa wachakataji huku akiahidi kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kuona namna ambavyo wadau hao watasaidika. 

Meneja wa Shamba la Miti la North Kilimanjaro ,Ersnest Madata amesema changamoto iliyopo kwa sasa ni mahitaji makubwa ya mazao ya misitu katika viwanda ukilinganisha na uwezo wa Shamba hilo.

Mapema katika kikao cha Wadau wa Misitu na wafanyakazi wa mashamba ya miti ya West Kilimanjaro na North Kilimanjaro wamiliki wa viwanda vya kuchakata mazao ya misitu na wanunuzi wa mazao hayo wakapata nafasi ya kutoa kero zao kwa naibu Waziri Kanyasu.

Mashamba ya Miti ya North Kilimanjaro na West Kilimanjaro yanaukubwa Heksri 15701 yakiwa yamepakana na nchi ya Kenya ,Wilaya ya Longido mkoani Arusha na Hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment

Pages