HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 10, 2013

AY AWATAKA WADAU WA ELIMU KUWAKUMBUKA WALIMU


Na Elizabeth John
MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini Ambwene Yessaya ‘AY’ ameomba wadau mbalimbali pamoja na Serikali kuhakikisha walimu wanapata huduma bora katika vitendea kazi na kuboreshewa mishahara yao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam na Habari Mseto Blog, AY alisema walimu wengi wapo katika mazingira magumu ya ufundishaji kutokana na baadhi yao kutokuwa na vifaa vya kufundishia hali ambayo inafanya kutotoa elimu bora kwa wanafunzi ambao nguzo kwa taifa.

“Nimepita katika shule nyingi na nimegundua kuwa wanachangamoto za vifaa vya kufundishia pamoja na ukosefu wa mishahara bora kitu ambacho kinatakiwa kufanyiwa kazi mapema ili kuhakikisha wanafunzi wanapata huduma bora na inayostaili,” alisema AY.

Pia nyota huyo alisema kuwa katika kipindi yuko katika harakati za kuachia kazi tofauti ili kuwaonesha wapenzi na mashabiki kuwa yuko katika hatua nyingine ya kimataifa ambayo inapaswa kuigwa na kila msanii ili kuhakikisha bendera ya Tanzania ina pepea vizuri katika anga za kimataifa kupitia muziki.

“Mashabiki wangu wakae mkao wa kula kutokana na kazi ambazo nimeziandaa kwa mwaka huu, baadhi yake ziko katika hatua za mwisho kukamilisha na moja ya kazi hiyo ni wimbo ambao mpya ninaoutarajia kuuachia Februari mwaka huu,” alisema AY.  

No comments:

Post a Comment

Pages