HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 11, 2013

JESHI LA POLISI LAWASHIKILIWA POLISI WATANO KWA TUHUMA ZA KUTOWEKA NA MILIONI 150 KATIKA TUKIO LA UJAMBAZI


DAR ES SALAAM, Tanzania 

JESHI la Polisi Kanda ya Dar es Salaam inawashikilia Polisi watano kwa tuhuma za kuhusika na upotevu wa sh. mil 150, tukio lililotokea Desemba 14 mwaka jana katika eneo la Kariakoo

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar esSalaam Jana Kamanda Kova, alisema alichounda yeye kwa wakati huo ni jopo la uchunguzi ambalo taarifa zake hazina ulazima wa kutolewa mbele ya jamii zaidi ya kutumika kwa ajili ya utekelezaji wa kile walichokibaini.

“Naomba mnielewe leo nimekuja na kile nilichorekodi wakati ule na mtasikiliza ila ninachoweza kuwaambia jopo halipewi hadidu za rejea na linaundwa na wataalam, tofauti na tume ambayyo hupewa hadidu za kitu wanachotakiwa kufanya na kisha majibu yake kupelekwa kwa jamii”alisema Kova.

Aliongeza kuwa baada ya kuunda jopo kwa wakati huo jukumu la kupeleleza sakata la Dk Ulimboka liliondoka mikononi mwake na kuwa chini ya ofisi ya  mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini(DCI) na kwamba kama kutakuwa na mswali yenye kumuhusu Dk Ulimboka ni vema waandishi wakawasiliana na ofisi ya Mkurugenzi huyo

Katika video hiyo inayoonyesha imefanyiwa marekebisho (Editing), Kamanda Kova anaonekana akiwa na askari wawili, mmoja akiwa na nyota tatu huku kukiwa na kinasa sauti cha kituo cha Televisheni ya  ITV peke yake katika eneo la kuwekea vinasa sauti.

Akizungumzia tukio la ujambazi lililotokea eneo la Kariakoo Desemba 14 mwaka jana Kova alisema, baada ya tukio hilo kulikuwa na taarifa kuwa askari waliopambana na majambazi walitoweka na mfuko wa fedha, hali iliyosababisha jeshi hilo kanda maalum kuunda jopo ya kuchunguza suala hilo.

Alisema dalili za awali zinaonesha kuwepo kwa hali ya ushiriki wa askari watano katika upotevu wa fedha hizo na kwamba askari hao wanashikiliwa huku uchunguzi zaidi ukifanyika.

Aliongeza kuwa askari wanaoshikiliwa ni wenye vyeo vya steshen staf sajent mmoja na wengine wannne wenye veo vya ukoplo.

Alisema askari hao kwa sasa watajibu mashtaka ya kijeshi kabla ya kufikishwa katika mahakma za kiraia.

Aidha Kamanda Kova, alisema mbali na askari hao pia wanawashikilia watu wengine wawili kuhudiana na tukio hilo ambapo aliwataja kuwa ni Deogratias Kimaro (30), mkazi wa Karakata na Kulwa Mwakabala (30), mkazi wa KijiweSamli

Wakati huo huo Kamanda Kova leo amelazimika kutumia ushahidi wa video, kukanusha kauli  iliyowahi kuandikwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini, kuwa aliunda tume katika sakata zima la kuchunguza utekwaji wa mwenyekiti wa jumuiya ya madaktari  Dk Stephen Ulimboka.

Mbali na kutumia video kukanusha suala hilo pia Kamanda kova aliomba suala lolote linalohusiana na Dk Ulimboka asiulizwe yeye kwa sasa kwa kuwa jukumu hilo limeshaondoka katika uwezo wake wa kazi na lipo kwa wakubwa wake kiofisi

No comments:

Post a Comment

Pages