HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 11, 2013

SENATOR JULIUS MISELYA AZUNGUMZIA MCHAKATO WA KATIBA MPYA



 DAR ES SALAAM, Tanzania

MWANASIA mkongwe nchini Senator Julius Miselya amesema hatarajii kupatika Katiba Mpya itakayolingana na matakwa ya wengi, kutokana maoni ya wananchi bila kuwepo rasimu ya kuwaongoza.

Akizungumza jijini Dar es Salaam hivi karibuni Miselya ambaye pia ni mwaasisi wa Chama Demokrasia (DP), siyo Mchungaji Christopher Mtikila kama inavyodhaniwa na wengi, alisema kinachofanyika hivi sasa ni kiini macho na kupoteza muda wa wananchi.

Alisema walichotakiwa kukifanya watawala ni kuandaliwa rasimu yenye mapendekezo kisha kuisambaza kwa wananchi, ambapo baada ya kuipitia ndipo wapendekeze kipi kiingizwe kwenye Katiba hiyo mpya.

Miselya alisema kwa utaratibu unaotumika wa kutoa maoni haoni kama una nguvu ya kubadili kile kinacholalamikiwa bali anaamini makusudio yatabaki yale yale ya kulinda serikali ya chama kilekile kilichoifikisha nchi hapa ilipo.

Aidha, hali hiyo ya kukosekana  rasimu hiyo inachangia wananchi kushindwa kabisa kutoa maoni yenye tija na badala yake kila mtu anajisemea kile anachokitaka binafsi.

“Kinacho nisikitisha hapa ni wananchi kuchangia maoni huku wakiwa hawajui hata katiba yetu ya zamani ina upungufu gani  au ina mazuri yepi, hili ni jambo litatuweka pabaya katika kupata maoni yenye ya msingi, ndiyo maana tunasikia baadhi ya wanawake  wakitoa maoni ya kutaka waolewe na wanaume wawili”alisema Miselya.

Miselya alisema hadi sasa ukiangalia maoni yanayotolewa yamekuwa hayalengi kulisaidia taifa hili, mwisho wake watawala watakutana wenyewe na kupitisha matakwa yao.

“ Mimi naona katiba itakayopatikana haitakuwa na mabadiliko bali itakuwa ile ile ya kulinda maslahi ya watu wachache kama ilivyo sasa”alisema Miselya.

Alisema kinachojitokeza hivi sasa ni  Tume hiyo ya mabadiliko ya Katiba kufujaji wa fedha nyingi zinazotokana na kodi za walala hoi kwa kitu ambacho matokeo yake yanafhamika.

No comments:

Post a Comment

Pages