HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 13, 2013

Thomas Mashali ashinda ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati kwa kumtwanga kwa KO Mkenya Benard Mackoliech


Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela akimvisha ubingwa wa Afrika Mashariki bondia Thomas Mashali baada ya kumpiga Bernad Mackoliech wa Kenya kwa KO
Na Elizabeth John
BONDIA Thomas Mashali juzi aliweza kuutetea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati kwa kumtwanga kwa KO Mkenya Benard Mackoliech, raundi ya 6 katika pambano lililofanyika ukumbi wa Friends Corner jijini Dar es Salaam.

Katika raundi za mwanzo, Mackoliech alianza vizuri kitu kilichozua minong’ono kwa watu, kwamba haiwezekani ubingwa uende nchi nyingine kabla ya raundi ya tano Mashali kuzinduka.

Katika mapambano ya utangulizi, Bakari Mohamed alishinda kwa pointi dhidi ya Godfrey Musa katika pambano la raundi nne, Amaduu Mwalimu walitoka sare na Cosmas Kibuga, Mwaite Juma akashinda kwa KO dhidi ya Frank Zagarino katika raundi ya tatu.

 Pambano hilo liliendeshwa na refarii Mark Hatia na  majaji walikua ni Kulwa makaranga,  Sakwe Mtulya na Fidel Hynes.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, ambaye alikua mgeni rasmi katika pambano hilo, tanzania kuna vipaji vya ngumi hii ni furaha kwa watanzania wote kama ubingwa umeendelea kubaki nyumbani.

“Nampongeza sana Mashali kwa kutwaa ubingwa huo kwa mara nyingine.Tanzania tuna vipaji sana vya ngumi, hivyo tuendelee kukuza vipaji vya hapa kwetu na sio kutoka nchi za wenzetu,” alisema Kenyela.

No comments:

Post a Comment

Pages