HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 10, 2013

Benki ya Azania yachangia kampeni ya saratani ya matiti


Mkurugenzi katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania, Godwin Seiya (kushoto) akikabihdi mfano wa hundl wa shilingi milioni tano kwa Mkurugenzi wa wa Huduma za Afya wa Hospitali ya Aga Khan Dr. Jaffer Dharsee (kulia) ikiwa ni mchango wa benki hiyo wa kusaidia kampeni ya saratani ya matiti inayolenga kujenga uelewa juu ya ugonjwa huo. (Na Mpiga Picha Wetu)
 Mkurugenzi katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania, Godwin Seiya (kushoto) akikabihdi  hundl ya shilingi milioni tano kwa Mkurugenzi wa wa Huduma za Afya wa Hospitali ya Aga Khan Dr. Jaffer Dharsee (kulia) ikiwa ni mchango wa benki hiyo wa kusaidia kampeni ya saratani ya matiti inayolenga kujenga uelewa juu ya ugonjwa huo. 
Mkurugenzi katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania, Godwin Seiya (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuchangia kampeni ya saratani ya matiti inayoongozwa na hospitali ya matiti. Katikati ni Mkurugenzi wa wa Huduma za Afya wa Hospitali ya Aga Khan Dr. Jaffer Dharsee.

Na Mwandishi Wetu   
                                                                            
BENKI ya Azania imetoa shilingi milioni tano kwa Hospitali ya Agha Khan zitakazosaidia kupiga jeki kampeni za kukuza uelewa wa saratani ya matiti. 

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya fedha hizo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Benki ya Azania katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (Hazina na Maendeleo ya Biashara) Godwin Seiya, alisema kuwa benki yake imejikita katika kusaidia masuala mbalimbali ya kijamii ikiwa sehemu ya mchango wa benki hiyo kwa jamii.

Bw. Seiya alisema kuwa benki yake imeamua kuunga mkono kampeni ya saratani ya matiti  ili kuwashawishi wanawake na jamii kwa ujumla kufanya uchunguzi wa ugonjwa huo ili kupunguza hatari kwa wanawake wengi kupata ugonjwa huo siku za usoni. 

“Taarifa zinaonyesha kuwa zaidi ya wanawake milioni moja na laki tano wanatatizo la saratani ya matiti. Tanzania ina jumla ya wagonjwa 1,307 wa saratani ya matiti. Sisi benki ya Azania tunaamini kuwa njia pekee ya kupunguza tatizo hili ni kupitia kampeni.

“Tunaamini kuwa kwa kutoa taarifa sahihi, waathirika wa saratani ya matiti wanaweza kupata matibabu mapema na kuongeza nafasi yao kuendelea kuishi.

 Leo hii tunachangia shilingi milioni tano kuunga mkono kampeni ya mwaka huu ambayo inalenga kukuza uelewa wa saratani ya matiti,” alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Afya wa Hospitali ya Agha Khan, Dkt. Jaffer Dharsee wakati wa hafla hiyo alisema kuwa kampeni ya mwaka huu inalenga kufanyia uchunguzi zaidi ya wanawake elfu tano nchi nzima .

Dharsee alisema kuwa kampeni za mwaka jana zilizofanyika katika mikoa ya Dar se salaam, Mtwara, Dodoma na Lindi zilitumia zaidi ya dola za kimarekani laki moja (Shilingi milioni mia moja na sitini) ambapo wanawake zaidi ya elfu tatu walifikiwa na kampeni katika mikoa hiyo minne.

“Tutaendelea na kampeni mwaka huu na lengo letu ni kuwafikia wanawake zaidi ya elfu tano nchi nzima mwaka huu. Pia tutajumuisha na uchunguzi wa saratani katika shingo ya kizazi mwaka huu. Tunaasa makampuni mengine ya biashara kuunga mkono kampeni hizi,” alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages