HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 03, 2013

NADAL, FERRER FAINALI MEXICAN OPEN LEO


ACAPULCO, Mexico

Nadal sasa anatarajia kupigana kuwania ubingwa wake wa 38 wa kwenye viwanja vya udongo kwa kumuumana na mpinzani wake Ferrer, ambaye ameshinda mechi 19 mfululizo katika michuano hii hapa Acapulco na sasa anasaka taji la tatu mwaka huu

NYOTA wa tenisi duniani, Rafael Nadal (pichani kulia) amemchapa Mhispania mwenzake Nicolas Almagro kwa seti mfululizo za 7-5 6-4  na kufuzu fainali ya michuano ya Mexican Open 3013.

Nadal, ambaye hivi karibuni alirejea viwanjani akitoka kuuguza majeraha ya miezi saba aliyokuwa akikabiliana nayo, sasa atacheza fainali na bingwa mtetezi wa michuano hii David Ferrer pia wa Hispania.

Mkali huyo ambaye ni bingwa mara 11 wa Grand Slam, alimaliza nafasi ya pili katika michuano ya Chile Open, kabla ya kuibuka bingwa wa Brazil Open wiki mbili zilizopita.

Nadal sasa anatarajia kupigana kuwania ubingwa wake wa 38 wa kwenye viwanja vya udongo kwa kumuumana na mpinzani wake Ferrer, ambaye ameshinda mechi 19 mfululizo katika michuano hii hapa Acapulco na sasa anasaka taji la tatu mwaka huu.

Kwa upande wake Ferrer, alifanya kazi ya ziada kuibuka mshindi na kutinga fainali kwa kumchapa Mtaliano Fabio Fognini kwa 6-3 6-7 (5) 6-1, katiika pambano lililodumu kwa masaa mawili na dakika 23.

Fainali ya Nadal na Ferrer inatarajiwa kupigwa leo Jumapili, huku kila mmoja akipewa nafasi sawa na mwingine kuweza kuibuka mbabe wa michuano hii.

BBC

No comments:

Post a Comment

Pages