HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 03, 2013

FERGIE: BAADA YA RYAN GIGGS, SASA RIO FERDINAND


MANCHESTER, England

“Itakuwa uwezekano wenye nguvu kuu. Nadhani alifanya mengi makubwa na ya kuvutia msimu uliopita. Alijiongoza yeye binafsi katika njia sahihi”

BAADA ya kufanikiwa kurefusha kwa miezi 12 mkataba wa Ryan Giggs, kocha wa Manchester United, Sir Alex Ferguson – sasa amegeukia kwa beki wa kati wa klabu hiyo, Rio Ferdinand ili naye asaini nyongeza ya msimu mmoja.

Giggs, jana alitarajiwa kuingia katiika dimba la Old Trafford kucheza mechi yake ya 1,000 akiwa na Man United, tangu alipoichezea mechi yake ya kwanza miaka 22 iliyopita.

Ferguson alisema jana kuwa, anatarajia kumuona Ferdinand, 34, akirefusha zama zake klabuni Old Trafford anakomaliza muda wake wa mkataba kiangazi hiki.

Bosi huyo wa United alisema: “Itakuwa uwezekano wenye nguvu kuu. Nadhani alifanya mengi makubwa na ya kuvutia msimu uliopita. Alijiongoza yeye binafsi katika njia sahihi.”

Aidha, Fergie, alienda mbali na kuzungumzia kiwango na maisha ya Giggs dimbani tangu kutua kwake mikononi mwake: “Kipi nitasema kuhusu Giggs ambacho bado sijawahi kusema?

“Ni mchezaji wa kustaajabisha, wa kipekee kwa kila mtu. Ryan ni mfano wa kuigwa kwa sisi sote. Kiwango chake alichoonesha mwaka huu na furaha yake ya mchezo, imeonesha ni kwa namna gani alikuwa na kila sababu ya kurefusha uwepo wake hapa.”

Kwa upande wake, Giggs alisema: “Najisikia vizuri, nafurahia soka langu kuliko kipindi chochote maishani na, kitu muhimu, najihisi kuwa na mchango mkubwa kwa timu.”

The Sun

No comments:

Post a Comment

Pages