HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 21, 2013

SIKU YA AFYA YA MACHO DUNIANI

 MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Naomi Nnko akishiriki kuimba na wanakwaya wa kikundi cha Magu One Theatre (MOT), wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya ya Macho Duniani yaliyofanyika juzi (19.4.2013) katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza. (Picha na Emmanuel Ndege)
 Baadhi  ya wazee wakazi wa Wilaya ya Magu wakiwa katika maadhimisho ya Siku ya Afya Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Magu, baada ya kufanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho ili kuwawezesha kuona tena. Kutoka kulia ni Weja Mfalasi, Constantine Mgana na Bujingwa Ngelela. 
 MKUU wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana akisalimiana na baadhi ya wazee ambao walifanyiwa upasuaji wa macho na kuwawezesha kuona tena katika maadhimisho ya Siku ya Afya ya Macho Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza.
 MKUU wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana (watatu kutoka kushoto) akiwa katika Chuo Cha Ualimu Mukidoma kilichoko wilayani humo, wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo. Wengine katika picha ni viongozi na wahadhiri wa chuo hicho
MKUU wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana, akiteta jambo na Mkurugenzi wa hoteli ya Bujora Point Swimming Pool & Lodge, Benjamin Mgonzwa, baada ya ufunguzi wa ukumbi wa kisasa wa hoteli hiyo iliyoko Kisesa, wilayani Magu katika mkoa wa Mwanza

No comments:

Post a Comment

Pages