HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 27, 2013

KAMPUNI YA ESG YAONESHA NIA YA KUWEKEZA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu


KAMPUNI ya Uwekezaji ya Afrika Kusini (ESG), imetenga dola milioni 600 kwa ajili ya kuwekeza nchini katika ujenzi wa miradi mikubwa ya barabara, Bandari, reli pamoja na kuongeza uzalishaji wa nishati ya umeme.

Akizungumza na viongozi wa taasisi za serikali katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam juzi, Mwenyekiti wa ESG, Simon Haliva alisema Tanzania inavivutio vingi ambavyo kama vikiendelezwa vinaweza kuleta maendeleo makubwa kwa wawekezaji na taifa kwa ujumala.

Alisema kutokana na miradi mbali mbali aliyoelekezwa na viongozi hao atajitahidi kuifanyia kazi ili kuhakikisha anaanza mpango huo haraka ili kuongeza uzalishaji nchini.

“Mimi na wenzangu tutakaa na kuipitia kwa makini miradi hii mliyotuarika na baada ya muda mfupi tutarudi ili kuwekeana mikataba mbali mbali ya miradi mlionayo kwaajili ya kuifanyia kazi” alisema Haliva.

Naye Afisa Mwandamizi wa uwekezaji kutoka Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC), Brendan Maro alibainisha kuwa ujio wa wawekezaji hao nimafanikio ya jitihada zai za kila siku katika uwajibikaji wa kuhakikisha miradi mbali mbali inawezeshwa na kuleta tija kwa taifa.

“Tunaamini wawekezaji watakuja kwa wingi kwa kuwa wengi wameonyesha moyo wa kutusaidia kwa kushirikiana na sisi katika shughuli mbali mbali za maendeleo kupitia miradi mbali mbali” alisema Maro.

No comments:

Post a Comment

Pages