HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 16, 2013

MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI APIGWA NA KUJERUHIWA VIBAYA

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari muda huu amepigwa na kujeruhiwa vibaya damu zinamtoka Puani, amepigwa na vijana wa kisomali, katika eneo la Zaburi kata ya Makuyuni Jimbo la Monduli, Taarifa za awali zinasema baada ya Nassari kuondoka na gari  jingine, waliokuwa wanafuatana naye walienda kujibanza sehemu.

 Kiongozi wa Chadema aliyetambulika kwa jina la Teddy Ndossi na dereva wa Nassari. Dereva wa Nassari Guardian  Palangyo amepigwa mdomoni amevunjwa meno mawili, na kwa sasa wamempiga Katibu wa Chadema wa eneo hilo anayeitwa Kilongola, wapo Kituo cha Polisi Makuyuni kutafuta msaada zaidi.

Picha na taarifa zaidi zitawajia baadae.

1 comment:

  1. Hii sasa ccm wamezidi sana... Na wanavuka mipaka kabisa

    ReplyDelete

Pages