HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 28, 2013

'TUPO WANGAPI' YA SUMA MNAZARETI, TUNDA MAN YAANZA KUTESA


Na Elizabeth John


WIMBO unaokwenda kwa jina la ‘Tupo Wangapi’ ulioimbwa na wakali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Suma Mnazareti na Tunda Man unafanya vizuri katika tasnia ya muziki huo kutokana na ujumbe uliobeba.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Suma alisema wakati anatunga mashairi ya wimbo huo, waliangalia hali halisi ya mapenzi ya wakinadada wa Kitanzania ambayo kila siku yanakua na sura mpya.

“Unajua kila msanii ana mashabiki wake hivyo naamini kutokana na kufanya kazi na Tunda kumenisababishia kuzoa mashabiki wengi ikiwa ni pamoja na kusimama kwa mashairi yake,” alisema Suma Mnazareti.

“Nashukuru kazi zangu zinapokelewa vizuri na mashabiki, kitu ambacho kinaniongezea uwezo wa kuendelea kuandaa kazi nyingi ili kuendelea kufurahisha jamii pamoja na kuielimisha kupitia fani hii,” alisema.

Alisema amekuwa akiumiza kichwa kila siku kwa ajili ya kutengeneza vitu vizuri vyenye ujumbe kwa jamii, lengo lake likiwa ni kutoka kimaisha kupitia muziki.

No comments:

Post a Comment

Pages