HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 23, 2013

APANDISHWA KIZIMBANI KWA KULAWITI MTOTO WA MIAKA 4

Na  Walter Mguluchuma, Mpanda Katavi

Fundi baiskeli  mmoja Mkazi wa  Mtaa wa Nsemlwa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  Athumani  Mussa (54) amefikishwa  katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumlawiti (kunajisi)  mdomoni mtoto wa miaka 4 baada ya kumdanganya  kumpatia mdoli wa kuchezea

Mtuhumiwa  alifikishwa  mahakamani hapo na kusomewa mashitaka na mwendesha mashitaka mkaguzi wa  msaidizi wa polisi Razalo Masembo mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa.

Mwendesha  mashika  aliimbia  mahakama kuwa  mshitakiwa Athumani Mussa alitenda kosa hilo hapo julai 24 mwaka huu majira ya saa 12 jioni nyumbani kwake katika Mtaa wa Nsemlwa mjini hapa.

Mtuhumiwa anadaiwa siku hiyo ya tukio  alimwona mtoto huyo akiwa na wenzake wakicheza barabarani karibu na nyumbani  kwake ndipo  alipo  mwita mtoto huyo na kumwambia amfuate  nyumbani kwake ili akampe mdoli wa kuchezea.

Mwendesha mashitaka aliendelea kueleza  kuwa  mara  baada ya mtoto huyo kuingia ndani mtuhumiwa  alianza kumlawiti  ( kumnajisi)  mtoto  huyo mdomoni huku akiwa amekaa kwenye kochi lake  sebuleni.

Ilidaiwa  licha  ya  mtoto  huyo kupiga mayowe ya kuomba msada mtuhumiwa   hakujali mayowe ya mtoto huyo bali aliendelea na shughuli yake  hadi hapo alipo maliza haja yake hiyo ya  kumlawiti mdomoni.

Mwendesha mashitaka  alidai kuwa  mtoto huyo  alipo  toka nyumbani kwa mtuhumiwa  alielekea   nyumbani kwa mama yake huku akiwa akilia  kwa sauti kubwa  hari iliyo pelekea watoto wenzake wamfuate kwa nyuma
.
Masembo alieleza  mara baada ya kufika kwa mama yake  na alipoulizwa  analia nini   mtoto huyo alitema mdomoni mbele ya mama yake mbegu za kiume  na kisha alimweleza mama yake kuwa amelawitiwa mdomoni na fundi baiskeli anaitwa  Mussa
Mama wa mtoto huyo baada ya kujua mwanae amelawitiwa mdomoni  alianza kuangua kilio na kufanya majirani wkusaniyike hapo   ndipo alipo waeleza mkasa huo aliofanyiwa    mwanae na mtuhumiwa.

Majirani hao ndio walipo chukua jukumu la kwenda kumkamata mtuhumiwa   wakiwa  wanaongozwa na mtoto huyo ambae  awali alikuwa amekataa kuingia ndani ya nyumba hiyo ya mtuhumiwa kwa kile alidai  anaogopa kulawitiwa tena  na mtuhumiwa
Mtuhumiwa   Athumani  Mussa alikana shitaka hilo  na  Hakimu Mkazi Mfawidhi Chiganga Ntengwa aliamuru mshitakiwa  apelekwe rumande  hadi hapo septemba 2 kesi yake itakapo  sikilizwa 

No comments:

Post a Comment

Pages