HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 31, 2013

CRDB, TFF KUELIMISHA MASHABIKI TIKETI ‘KIELEKTRONIKI’
Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka tanzania (TFF), Boniface Wambura akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu elimu watakayotoa kwa mashabiki wa soka juu ya mfumo mpya wa matumizi ya tiketi za kielekroniki. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi TFF, Salum Madadi.
DAR ES SALAAM, Tanzania

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), kwa kushirikiana na Benki ya CRDB, wamejipanga kutoa elimu kwa mashabiki wa soka nchini juu ya mfumo mpya matumizi ya tiketi za Kielektroniki zinazotarajiwa kuanza kutumika rasmi katika raundi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

CRDB ndio wazabuni walioshinda tenda ya kuuza aina hiyo ya tiketi, ambazo mpaka sasa zimeanza kufanyawiwa majaribio ya mauzo katika mechi ya Azam FC, dhidi ya RuvuShooting kwenye Uwanja wa Chamazi wiki iliyopita.

CRDB kwa kushirikiana na TFF, leo inatarajia kuendelea na mxchakatop wa majaribio ya mauzo ya tiketi, kupitia pambano la kirafiki maalum kwa ajili baina ya Ashanti United dhidi ya Maafande wa JKT Ruvu.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema hayo leo kuwa, wameamua kufanya hivyo kutokana na uelewa mdogo wa baadhi ya mashabiki wa soka, uliodhihirika na mechi ya awali ya majaribio ya tiketi hizo.

Wambura alisema, elimu hiyo itatolewa kwa kina, kwani wamegundua watu hawajui nini maana ya tiketi hizo kwani katika mchezo uliopita walipata wakati mgumu juu ya suala hilo.

“Mchezo uliopita dhidi ya Azam FC na Ruvu Shooting, TFF na CRDB tulipata wakati mgumu mara baada ya mashabiki kuja na pesa zao uwanjani wakijua tiketi hizo zinapatikana pale moja kwa moja - wakati sio hivyo,” alisema Wambura.


Aliongeza kuwa, TFF inaangalia uwezekano wa kuwapa semina waandishi wa habri ili waweze kufikisha ujumbe kwa umma juu ya matumizi sahihi ya mfumo huo wa tiketi za kielektroni.

No comments:

Post a Comment

Pages