HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 23, 2013

DK. NDUGULILE:TUMIENI MICHEZO KUJIEPUSHA NA DAWA ZA KULEVYA
Mbunge wa Kigamboni Dk Faustine Ndugulile amesema vijana wakitumia michezo ipasvyo watajiepusha na janga la matumizi ya dawa za kulevya.


Dk Ndugulile alitoa kauli hiyo jana Mbagala jijini Dar esSalaam katika sherehe ya kutimiza mwaka mmoja wa klabu ya mazoezi ya Mbagala Jogging.

Alisema kwa nafasi yake ya udaktari wa binadamu anafahamu umuhimu wa mazoezi katika mwili wa binadamu hasa katika kupunguza vichocheo vinavyowaingiza vijana katika tabia zisizostahili.

Mnaweza kujiepusha katika matumizi ya dawa za kulevya kwa kufanya mazoezi na mkidanikiwa katika hili mtakuwa mmejiepusha kwa kiasi kikubwa na maradhi ya ukimwi kwani kwa takwimuza manispaa yaTemeke kila wanawake watatu wanaojichoma sindano za dawa ya kulevya wawili kati yao wameathirika kwa ugonjwa wa ukimwi,huku katika kila wanaume watatu wenye kujidunga mmoja ameathirika

Kuhusu vijana kujiunga pamoja alisema wanaweza kutumia fursa hiyo kuanzisha miradi itakayofadhikiwa na serikali

Katika maadhimisho hayo ya klabu ya mbagala Joging zaidi ya vilabu 40. kutoka manispaa ya Temeke walishiriki kufanya mazoezi ya pamoja.

MBUNGE wa Kigamboni Dk Faustine Ndugulile akiwaongoza wananchi mbali mbali wa wilaya ya Temeke waliojitokeza kushiriki sherehe ya  kutimiza mwaka mmoja kwa klabu ya mazoezi ya Mbagala, vijana na wazee walishiriki katika joggin kabla ya hotuba ya mbunge huyo.
Wakifanya mazoezi ya viungo.






Dk. Ndugulile akikata keki kuashiria kutimia kwa mwaka mmoja wa  klabu ya Mbagala Jogging.
Mdau wa Mbagala Joggin kutoka gazeti la Tanzania Daima Abdallah Khamis akilishwa keki  katika sherehe hizo.
Moshi Lusonzo kutoka  gazeti la Nipashe linalomilikiwa na makampuni ya IPP naye alishiriki katika keki ya kutimiza mwaka mmoja kwa klabu ya Mbagala Jogging.
Dk Ndugulile akiwa na wanamichezo kutoka klabu ya Mbagala Jogging.

No comments:

Post a Comment

Pages