HABARI MSETO (HEADER)


June 29, 2014

FID Q: MASHAIRI YANGU NATOA KWA BABU


Na Elizabeth John
MKALI wa hip hop nchini, Farid Kubanda ‘Fid Q’ amesema asilimia kubwa ya misemo ya mashairi yake huwa anaitoa kwa babu yake na baadhi ya vitabu vya hadithi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, Fid Q alisema, babu yake ni muongeaji sana na akikaa naye kuwa anakariri maneno mengi ambayo yanamsaidia katika utunzi wa mashairi yake.

“Babu yangu amenisaidia sana mpaka kufika hapa, namsdhukuru sana, pia msanii umatakiwa kusoma vitabu mbalimbali ili kupata baadhi ya maneno ambayo yataleta vionjo katika mashairi yako,” alisema.

Fid Q alisema kwasasa yupo katika mikakati ya kuandaa kazi yake mpya ambayo anaamini itakuwa moto wa kuotea mbali kutokana na mashairi ambayo yapo ndani yake.

Msanii huyo ni kati ya wasanii wakongwe ambao wanatamba katika tasnia hiyo akiwa na kazi zake kama ‘Agosti 13’, ‘Siri ya Mchezo’, ‘Mwanza Mwanza’ na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri.

No comments:

Post a Comment

Pages