HABARI MSETO (HEADER)


June 29, 2014

RIYAMA AKILI MAPUNGUFU YA LUGHA KWA WASANII


Na Elizabeth John
STAA wa filamu za Bongo, Riyama Ally amesema lugha ya Kingereza ni tatizo kubwa kwa wasanii wa Bongo inayopelekea kushindwa kutamba kimataifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Riyama alisema hakuna mtu ambaye atapingana nay eye kwa hilo, wasanii wengi wamekuwa wakifanya vizuri hapa nchini lakini wanapokwenda huko wataboronga.

“Mimi binafsi ukinipeleka nchi za watu hakika utakuwa na kazi ya ziada ya kunifafanulia anachokiongea, wengi sio wawazi mimi siwezi kucheza na mtu anayeongea lugha nyingine nitawasiliana nae vipi sasa,” alisema Riyama.

Aidha, Riyama alisema kwasasa akitokea mtu anayetaka kumsomesha ili kuendeleza kipaji chake yupo tayari wakati wowote na anahamu ya kujua lugha nyingine.

Riyama ni kati ya walimbwende wanaotamba katika tasnia ya filamu nchini huku akishiriki filamu nyingi zikiwemo, Kigodoro, Tabu ya kuoleana, Fungu la kukosa, Wrong Number na nyinginezo nyingi ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages