HABARI MSETO (HEADER)


June 27, 2014

NSSF YATOA MAFUNZO KWA WAJASIRIALI WANAWAKE WA EOTF
Ofisa Mwandamizi wa NSSFkutoka Kitengo cha Hiari Scheme, Salim akiwa na cheti cha ushiriki wa mafunzo  ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wanawake alichokabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kulia), wakati wa kufunga mafunzo hayo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF), Mama Anna Mkapa. 

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limewataka watanzania kutumia fursa zinazotolewa na mfuko huo ili kujikwamua  kiuchumi kwa kupata akiba , mafao na mikopo itakayo kuwa sawa na watu walioajiriwa.

Akitoa rai hiyo jijini Dar es Salaam,  Ofisa Mwandamizi kutoka Kitengo cha Hiari Scheme, Salim Kimaro wakati wa Kufunga Mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake wajasiriamali waliotoka katika mikoa yote ya Tanzania.

Alisema kuwa, ili kuhakikisha kila mtu anafaidika na mfuko huo wamelenga kupanua wigo kwa watanzania wote ili wanufaike na  huduma wanazotoa  ikiwemo Pensheni, mafao ya mtibabu na uzazi kama ilivyo kwa watu walioajariwa.

“Nchi yetu inakadiriwa kuwa na watu Millioni 44, ambapo nguvu kazi ya watu wa umri kati ya miaka (15-60) ni million 22.7,  kati yao million 1.2 tu ndio wanahudumiwa na mfuko wa Hifadhi ya Jamii,  hii inamaanisha watu million 21.6 ndio walioko katika ajira binafsi na hawafikiwi na Mfuko wa hifadhi ya Jamii hivyo tumeona ni bora kuhusisha sekta binafsi ili kuwakomboa watanzania”

Alifafanua sababu ya kuhusisha sekta binafsi katika hifadhi ya jamii kuwa ni,  kutoa mafao yote yanayotolewa na NSSF, kusaidiana na serikali kupunguza umasikini, kuwajengea uwezo wajasiriamali kwa kuwapa mikopo, kuwapa wanachama huduma ya matibabu bure ili waweze kupata afya na kuendelea kuzalisha mali.

“Ili kuwa mwanachama wa hiyari unashahuriwa kwenda ofisi yoyote ya  NSSF iliyo karibu nawe isipokuwa makao makuu, ambapo mtu anatakiwa kutoa tamko la kipato chake kwa mwezi ili kutoa asilimia 20, pia mwanachama wa hiyari au sekta binafsi atapaswa kulipa kiwango chochote kisiwe chini ya sh 20, 000 kila mwezi”


Kimaro alisema kuwa miongoni mwa faidia na mambo muhimu watakayowanufaisha wanachama ni kutoa mikopo ya elimu, uendelezaji wa biashara na kuboresha makazi, matibabu ya bure kwa wanachama na familia zao (mke, mume na watoto wane wa chini ya miaka 18-21 iwapo wako shule).


Aliongezea kuwa “Mwanachama wa hiari anayo haki ya kupata mafao yote saba yatolewayo na NSSF kwa mujibu wa sheria, mafao hayo ni ya muda mrefu yaani Pensheni ya uzee, urithi na ulemavu na mafao ya muda mfupi  ambayo ni matibabu, uzazi, kuumia kazini na msaada wa mazishi”

No comments:

Post a Comment

Pages