NA ELIZABETH JOHN
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Omary Nyembo ‘Ommy
Dimpoz’ amesema mashairi aliyoimba katika wimbo wa ‘Nani Kama Mama’
alioshirikishwa na Christian Bella aliandika akiwa anamaanisha.
Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, wakati wa shoo hiyo
ambayo iliandaliwa maalum kwaajili ya wimbo huo ikijulikana kama ‘Usiku wa Nani
Kama Mama’, alisema anatamani mama yake angekuwepo angeona mafanikio
aliyoyapata kupitia muziki.
“Mama yangu alitangulia mbele za haki, huwa natamani sana
angekuwepo ili aone mafanikio niliyoyapata kupitia muziki kama wengine
wanavyoona mafanikio ya watoto wao, mashairi ya wimbo huu nilikuwa namanisha
sio wimbo ni maneno ambayo yapo na kila siku huwa namuombea apumzike salama,”
alisema nyota huyo kwa uchungu.
Dimpoz aliwataka wasanii ambao wamekuwa wakipata mafanikio
na wazazi wao wakishuhudia, kuwajali na kuwatunza kwa moyo wote kwasababu ndio
chanzo cha mafanikio yao.
Dimpoz kwasasa anatamba na ngoma yake ya ‘Ndagushima’
ambayo inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio licha ya kuwa na kazi
nyingi ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri.
No comments:
Post a Comment