NA
ELIZABETH JOHN
BAADA ya kutajwa kuwania tuzo za IRAMWA
(International Reggae and World Music Awards), za nchini Marekani, nyota wa
muziki wa kizazi kipya nchini, Nasseb Abdul ‘Diamond Platinumz’ ameomba wadau wa
muziki huo kuendelea kumpa sapoti.
Mtanzania mwingine aliyetajwa katika
tuzo hizo ni msanii wa dancehall, Dabo ambaye ametajwa kuwania tuzo hizo katika
kipengele cha 'Best New Entertainer'.
Diamond alitajwa kuwania tuzo hizo
kupitia ngoma yake ya ‘Mdogo Mdogo’ katika kipengele cha 'The Best African
Song/Entertainer' akichuana na mkali kutoka Nigeria, Davido kupitia ngima yake
ya ‘Aye’, Awilo Longomba (Bendeke), Willy Paul Msafi (Tam Tam), Eddy Kenzo
(Sittya Loss), na Bracket (Mama Afrika).
Diamond ambaye sasa yupo nchini
Marekani alipoalikwa kutumbuiza, kupitia mtandao wake wa Instagram aliandika
kuwa sapoti ya Watanzania ni muhimu kumuwezesha yeye kuchua tuzo hiyo. Upigaji kura tayari umeshafunguliwa na
tuzo hizo zitatolewa Oktoba 4, mwaka huu nchini Marekani.
Hivi karibuni Diamond alipeperusha
vizuri bendera ya Tanzania kwa kunyakua tuzo ya AFRIMMA mwaka huu zilizofanyika
Julai 26, Eisemann Center Richardson, Texas nchini Marekani
akichaguliwa Mwanamuziki Bora wa Kiume Afrika Mashariki.
No comments:
Post a Comment