Na Mwandishi Wetu, Tanga
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union “Wagosi Kaya “umekanusha vikali taarifa
zilizoenezwa kuwa mlinda mlando wa kikosi cha Vijana wenye umri
chini ya miaka ishirikini U-20 Fikirini Suleimani “Mapara kuwa amesajiliwa na
Klabu ya African Sports “Wanakimanumanu”
Taarrifa
hizo hazina ukweli wowote bali Fikirini bado ni mchezaji halali wa
Klabu ya Coastal Union ya Tanga na ni miongoni mwa wachezaji
watakaoonekana kwenye kikosi hicho msimu ujao.
Taarifa iliyotolewa leo kwa nyombo vya Habari kupitia msemaji wa Klabu
hiyo Oscar Assenga zimeelezwa kuwa fikirini bado ana ni mchezaji halali wa timu
hiyo kwa kusajiliwa hivyo tarifa ya kuwa amejiunga na Africa Sports hazina
ukweli wowote ule.
Assenga amesema kuwa ili wadau wa
soka waweze kuthibitisha kuwa mchezaji huyo bado yupo kwenye kikosi cha wagosi
hao wa kaya wafike mazoezini Jumatatu kwani atakuwepo kwenye mazoezi hayo.
Amesema kuwa Fikirini ni miongoni mwa wachezaji waliosajiliwa kwa ajili
ya kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa Ligi kuu soka Tanzania bara.
No comments:
Post a Comment