Na Mwandishi Wetu
Aliyekuwa Kocha wa makipa wa timu ya Yanga Razack Siwa hatimaye ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu ya Coastal Union ya Tanga ambayo inajiandaa na maandalizi ya msimu ujao wa Ligi kuu Tanzania Bara utakaoanza mwezi Septemba. Siwa ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja lengo likiwa kuipa mafanikio makubwa timu hiyo msimu ujao.
Tayari Kocha Siwa ameungana na wachezaji wa timu hiyo leo kupanda ndege kuelekea Visiwani Pemba ambapo timu hiyo inakwenda kuweka kambi ikijiwinda na michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.
Aliyekuwa Kocha wa makipa wa timu ya Yanga Razack Siwa hatimaye ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu ya Coastal Union ya Tanga ambayo inajiandaa na maandalizi ya msimu ujao wa Ligi kuu Tanzania Bara utakaoanza mwezi Septemba. Siwa ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja lengo likiwa kuipa mafanikio makubwa timu hiyo msimu ujao.
Tayari Kocha Siwa ameungana na wachezaji wa timu hiyo leo kupanda ndege kuelekea Visiwani Pemba ambapo timu hiyo inakwenda kuweka kambi ikijiwinda na michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.
Akizungumza kabla ya timu hiyo
kuondoka, Katibu Mkuu wa Coastal Union, Kassim El Siagi amesema kuwa
kocha huyo wa makipa anachukua nafasi iliyokuwa wazi kutokana na kutokuwa na mwalimu
maalumu wa kuwafundisha walinda milango wa Coastal Union.
Akizungumzia
safari ya timu hiyo, El Siagi alisema kuwa safari ya timu hiyo leo
wameondoka wachezaji 27 wakiaambana na walimu wa timu hiyo ambao
wameondoka ambapo watakapofika pemba watafanya mazoezi kwenye uwanja wa soka
Gombani.
Safari hiyo imefadhiliwa na wadhamini wa timu
hiyo kiwanda cha Pemba Floor Mills kilichopo mjini Tanga ambao wamedhamiria
kuhakikisha wanaipa mafanikio timu hiyo.
Katibu huyo amesema wakiwa visiwani
humo watacheza mechi nne za majaribio ambazo zilikwisha kutayarishwa na chama
cha mpira wa miguu Pemba pamoja na kuwataka mashabiki na wapenzi wa timu hiyo
kuacha kuwa na wasiwasi na timu hiyo kwa sababu wamefanya usajili wa nguvu .
No comments:
Post a Comment