NA KENNETH
NGELESI, MBEYA
SIKU chache
baada ya Mbeya City kurejea kutoka Mikoa ya Rukwa na Katavi iliko kuwa kusaka
vipaji na makali ya kujiwinda na Ligi
kuu Tanzania Bara, kakazao na wapinzani wao wakuu Tanzania Prisons nao
wanondoka leo kuelekea Mjini Sumbwanga kwa ajili ya kucheza michezo ya kirafiki.
Taarifa ya iliyotolewa
na Meneja wa timu hiyo Enock Lupwuto na kwamba wanaenda mjini Sumbawana Mkoani Rukwa baada ya kupata Mwaliko
na chama cha Soka Mkoa huo (RUREFA).
Akizungumza
na Tanzania daima jana Meneja huyo alisema kuwa safari itaanza leo majira ya sabui kwa basi la timu
hiyo na kwamba wakiwa mjini Sumbawanga wanacheza mechi mbili ya kwanza itakuwa
dhidi ya Kombain FC mchezo ambao utapigwa leo katika dimba la Nelsoni Mandela.
Lupwuto
alisema kuwa mbali na mchezo huo wa leo timu hiyo itashuka dimbani jumapili,kwa
kucheza na timu ambayo watapangiwa na wenyeji wao, chama cha soka Mkoa wa
Rukwa.
Meneja huo
aliongeza kuwa baada ya timu yao kufanya vibaya katika msimu uliopita ambapo
ilimaliza ikiwa nafasi ya kumi na moja,safari hiii wamedhamiria kufanya vizuri
zaidi ikiwa ni pamoja na kuchukua ubingwa msimu.
Tanzania
Prisons iliyo panda daraja mwaka 1995 na mwaka 1999 ilichukua ubingwa wa ligii
kuu,itaondoka leo msafara huo utakuwa na
wachezaji 27 na viongozi 5 kitajereaji
jiji Mbeya Semtemba mosi
Alisema kuwa
mara baada ya kurejea jiji Mbeya, msafara huo juma tano Semptemba 3 itaondoka kuelekea jiji
Dar es Salaamu ambapo itacheza michezo kadhaa ya kirafiki kabla ya ligi kuu
kuanza kutimua vumbi Semptemba 20 mwaka huu.
Tanzania Prisons inayo nolewa na Devid Mwamwaja inafanya ziara
hiyo ikiwa ni siku kadhaa tangu wawakilishi wengine kutoka Mbeya,Mbeya Cit FC
kurejea kutoak Mikoa ya Rukwa na Katavi ilicheza michezo mitatu ikitoka sare 1
na miwili kushinda.
No comments:
Post a Comment