HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 20, 2015

SHETA KUMPA ZAWADI YA GARI MKE WAKE


NA ELIZABETH JOHN

BAADA ya kugombana na mkewe, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nurdin Bilal ‘Shetta’ amesema kuwa, endapo kama mkewe atarudi nyumbani amemuandalia zawadi ya gari aina ya Mark X.

Mke wa Shetta (mama Kaila), aliondoka nyumbani kwake baada ya msanii huyo kudaiwa kulala chumba kimoja na msanii wa filamu nchini, Rose Ndauka mjini Morogoro walipokwenda kwenye msiba wa aliyekuwa muasisi wa Top Top Connection, marehemu Abdul Bonge.

Akihojiwa na Clouds FM, Shetta alisema kuwa, mkewe hataki kabisa kumuelewa kuhusu suala hilo na sasa hivi anadai taraka akisema kwamba uhusiano wao ubaki kwa kumhudumia mtoto tu.

“Yani hataki kabisa kunielewa, nafikiri kuna mtu ambaye anampa maneno ya uongo lakini kiukweli kabisa mke wangu bado nampenda sana tu sijui kwa nini hataki kunielewa maana nimefanya vitu vingi kanielewa na endapo akirudi nimeandalia gari la kutembelea yeye pamoja na mtoto,” alisema.


Shetta kwa sasa anatamba na ngoma yake ya ‘Shikorobo’ ambayo amemshirikisha nyota kutoka Nigeria, KCEE.

No comments:

Post a Comment

Pages