HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 11, 2015

Mwandishi ajitosha ubunge jimbo la Mbeyua vijijini.

Mwandishi wa Habari, Gordon Kalulunga akizungumza na wananchi katika viwanja vya mahubiri Mjini Mbalizi wakati akitangaza nia ya kugombea Ubunge jimbo la Mbeya vijijini (Picha na Kenneth Ngelesi)

NA KENNETH NGELESI, MBEYA

MWANDISHI wa habari wa gazeti la Mtanzania kutokaMbeya, Gordon Kalulunga amejitosa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo la Mbeya vijijini kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM).

Kalulunga ambaye pia ni mlimikio wa Blog ya Kululunga Blog alitangaza kuingia kwenye mchakato wa kugombea kuteuliwa na Chama ili aweze kupeperusha bendara katika uchaguzi mkuu ujao kwwenye mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jana kwenye viwanja vya mahubiri Mbalizi mkoani Mbeya.

Mtia nia huyo alisema endapo Chama chake kitampitisha na hatimaye kushinda Ubunge katika Jimbo hilo atahakikisha wananchi wote wanajiunga na mfuko wa bima ya afya kwa ajili ya matibabu kwa kila kaya kuchangia ili kupunguza adha na gharama kubwa za matibabu.

Aliongeza endeapo atafanikiwa kuukwaa Ubunge  atahakikisha anasimamia na kupigania jimbo hilo liweze kupata chuo cha fani yoyote ili kuwawezesha ajili ya vijana kupata elimu jambo lilatalopunguza wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana.

Kalulunga alisema kipaumbele kingine atakachoshughulikia ni pamoja na kupigania ujenzi wa ofisi za makao makuu ya Wilaya hiyo katika eneo husika ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi tofauti na ilivyosasa ambapo Ofisi za Wilaya ya Mbeya zipo katikati ya Jiji la Mbeya.

Awali Katibu wa Umoja wa vijana chama hiccho Wilaya ya Mbeya vijijini (UVCCM),Japheti Siulanga aliwataka vijana wamuunge wamuunge mkono kijana mwenzao aliyejitokeza na kuonesha nia ya kutaka kuongoza akiwa Mbunge wa jimbo hilo.

Aidha katika mkutano huo vijana zaidi ya 26 walijiunga na Chama cha mapinduzi na kukabidhiwa kadi za umoja
wa Vijana.

No comments:

Post a Comment

Pages