HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 13, 2015

Njaa yawachomoa Magaidi msituni

Na Bryceson Mathias, Kibundu

MAGAIDI waliojificha ndani ya Msitu wa Kata ya Kibindu, mpakani mwa Bagamoyo, Kilindi na Mvomero, kwa sasa wanaathirika na Njaa, jambo ambalo linawafanya wang’oke msituni walikojificha na kwenda kwenye Makazi ya Wananchi kujipatia Chakula kunusuru Maisha yao.

Hatua ya Magaidi hao kuathiriwa na Njaa, inatokana na Wananchi kwenye Migahawa ya Mama Lishe na Baba Lishe, kutowauzia Chakula au Vitafunio watu ambao hawawatambui kama ambavyo awali kwa kutojua, walikuwa wanawauzia Maandazi yalikuwa yakikusanywa hadi kufika Gunia.

Wakati Magaidi hao wakihangaishwa na Njaa msituni humo, pia zipo taarifa za Kamati Tatu za Ulinzi za Wilaya Jirani kufanya Kikao cha Ujirani Mwema cha Wilaya Jirani, Mvomero, Bagamoyo na Kilindi, ili kupanga Mikakati thabiti ya kuwadhibiti Magaidi hao wakishirikiana na Wananchi.

Mmoja wa Viongozi wa Kamati hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini kutokana na   Kikao hicho kuwa ni cha Siri alisema, ”Ni kweli kuna Kikao cha Ujirani Mwema wa Kamati Tatu za Ulinzi na Usalama, za Mvomero, Bagamoyo na Kilindi, lakini yanayojiri ni Siri hayasemwi.

“Tunawataka Wanaowafadhiri na kuthubutu Kuwaficha Magaidi hao majumbani mwao, ambao ni Vijana Wadogo wadodo, Watoe taarifa Polisi au kwa Viongozi wa Vijiji, na ikibidi Magaidi wenyewe, Wajisalimishe wenyewe mapema, kabla hawajakumbana na Vyombo wa Dola”alisema Mtoa habari.

Habari Mseto Blog lilimtafuta Mtendaji wa Kijiji cha Kibindu, Juma Mgaza, kwenye simu ili kujua hali ya Usalama tuka kwenye Kijiji chake, lakini alijibu kwa Maneno ya Mkato, na kusema,  “Samahani niko kwenye Kikao”.

Hata hivyo, alipotafutwa aliyekuwa Diwani wa Kata hiyo, Mawazo Mkufya, kujua hali ya Ugaidi ikoje katika Kata ya Kibindu alisema, “Ni kweli Adui yako Muombee Njaa! Hali sasa ni Shwali, hapa tuna Askari wanaolinda Usalama na kupokea taarifa mbalimbali toka kwa Wananchi kuwahusu Magaidi hao, lakini hatubweteki, tuko Ki-Ulinzi zaidi”.alisema Mkufya.

Kwa Upande wake Mtendaji wa Kitongoji cha Pera, Mwanahawa Mabwani, alipoulizwa hali kwake ikoje alisema, “Pamoja na kwamba hali kwa sasa ni shwali, anakamatwa mtu mmoja mmoja,“Nimeamua kujiunga na Mafunzo ya Mgambo yanayoendelea hapa, ili niwe Mkakamavu”.alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages