HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

October 11, 2015

BENKI YA CRDB YAADHIMISHA KILELE CHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto) akikata keki na mmoja wa wateja wa Benki hiyo tawi la Oysterbay wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja iliyofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. (Picha na Francis Dande)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akimlisha keki mmoja wa wateja waliofika kupata huduma katika tawi la CRDB Oysterbay jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki, wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja. Kushoto ni Meneja wa Benki hiyo tawi la Oysterbay, Juliana Mhimbira.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akimlisha keki mmoja wa wateja waliofika kupata huduma katika tawi la CRDB Oysterbay kama ishara ya kuwashukuru wateja wa Benki hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja iliyofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto) akisikiliza maoni ya mteja mkubwa wa Benki ya CRDB tawi la Oysterbay jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki, wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza na wateja wa Benki ya CRDB tawi la Oysterbay jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki, wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB akipokea zawadi ya maua kutoka kwa Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Lumumba Upendo Assey wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
 Dk. Charls Kimei akisalimiana na wateja.
 Dk. Charles Kimei akizungumza na wateja wa Benki ya CRDB.
 Dk. Kimei akizungumza na waandishi wa habari.
 ‘Tumerejesha bil. 1.3/- kwa jamii’

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei amesema benki yake imetumia sh bilioni 1.3 ikiwa ni sehemu ya faida yake, kurejesha kwa jamii kupitia sekta ya elimu, afya na mazingira.

Alizungumza hayo akiwa na baadhi ya wateja wa benki hiyo Tawi la Oysterbay mwishoni mwa wiki wakati wa hitimisho la Wiki ya Huduma kwa Wateja wa CRDB nchini kote.

“Oktoba ya kila mwaka tunatumia wiki hii kurejesha asante yetu kwa jamii, tumegawa madawati katika shule mbalimbali za msingi yenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 40 kwa shule mbalimbali za msingi hapa nchini.

“Manispaa ya Kinondoni tumepeleka dawa na vitendanishi kwa ajili ya kipindupindu vyenye thamani ya sh. milioni 15 pamoja na shughuli nyingine nyingi zilizofanywa na watumishi wetu kwenye matawi yetu yote,” alisema Dk. Kimei.

Alisema umuhimu wa wiki ya huduma kwa wateja ni kuboresha ufanisi wa utendaji na huduma kwa kuwa ni kipindi cha wateja kueleza kero, maoni na ushauri wao kwa uwazi.

Wiki ya huduma kwa wateja wa CRDB huadhimishwa kuanzia Oktoba 5 hadi Oktoba 11 ya kila mwaka ambapo wafanyakazi wa benki hiyo hufanya shughuli mbalimbali za kijamii.

No comments:

Post a Comment

Pages