HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 17, 2015

Ecobank Tanzania yakarabati hospitali ya Ligula-Mtwara

Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Mtwara Bi. Fatma Ally (katikati) akiwasili kwenye hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank ambayo ilifanyika mkoani Mtwara kitaifa. Katika kusherekea siku hii, wafanyakazi wa benki hii barani Afrika huhamasishwa kujitolea muda wao kwa ajili ya shughuli za kijamii zenye manufaa kwa jamii husika. Ecobank Tanzania ilisherekea siku hii kwa kukarabati moja ya wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Ligula mkoani Mtwara.
Mkurugenzi mkuu wa Ecobank Tanzania Bw. Enoch Osei-Safo akimkaribisha Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara Bi. Fatma Ally ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Mtwara katika hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank ambayo ilifanyika mkoani Mtwara mwishoni mwa juma. Katika kusherekea siku hii, wafanyakazi wa benki hii barani Afrika huhamasishwa kujitolea muda wao kwa ajili ya shughuli za kijamii zenye manufaa kwa jamii husika. Ecobank Tanzania ilisherekea siku hii kwa kukarabati moja ya wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Ligula mkoani Mtwara.

Mkurugenzi Mkuu wa Ecobank Tanzania Bw. Enoch Osei-Safo akiwasalimia wakazi wa mkoa wa mtwara (hawapo pichani) katika hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank ambayo ilifanyika mkoani Mtwara mwishoni mwa juma. Benki ya Eco Tanzania ilisherekea siku hii kwa kukarabati moja ya wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Ligula mkoani Mtwara ambapo walichangia kiasi cha dola za kimarekani elfu kumi na tano.

Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Mtwara Bi. Fatma Ally (katikati) akitoa hotuba yake katika hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank ambayo ilifanyika mkoani Mtwara mwishoni mwa juma. Katika kusherekea siku hii, wafanyakazi wa benki hii barani Afrika huhamasishwa kujitolea muda wao kwa ajili ya shughuli za kijamii zenye manufaa kwa jamii husika. Ecobank Tanzania ilisherekea siku hii kwa kukarabati moja ya wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Ligula mkoani Mtwara.
Baadhi ya wafanyakazi wa Ecobank Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja na watoto wa mkoa wa Mtwara wakati wa hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank ambayo ilifanyika mkoani Mtwara mwishoni mwa juma. Katika kusherekea siku hii, wafanyakazi hao walijitolea kufanya shughuli za kijamii ambapo walishiriki katika ukarabati wa moja ya wodi ya watoto katika hospitali ya Rufaa ya Ligula mkoani Mtwara.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Mtwara Bi. Fatma Ally akikagua wodi ya watoto katika hospitali ya mkoa na rufaa ya Ligula mkoani Mtwara ambayo benki ya Ecobank Tanzania ilijitolea kukikarabati wakati wa hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank ambayo ilifanyika mkoani humo mwishoni mwa wiki.

Kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara Bi. Fatma Ally (wa pili kulia) akipata maelezo ya utaribu mzima wa ukarabati wa wodi ya watoto katika hospitali ya Ligula kutoka kwa Meneja wa tawi la Ecobank-Mtwara Bw. Davis Minja (wa kwanza kushoto). Benki yaEcobank Tanzania ilijitolea kukarabati wodi hiyo ya watoto wakati wa hafla ya kuadhimisha siku ya Ecobank. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo hapa nchini Bw.Enoch Osei-Safo.

No comments:

Post a Comment

Pages