HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 21, 2015

KAMPENI YA NSSF KWANZA YAWAFIKIA WATU WENGI MKOANI MBEYA

Wananchi wa Kijiji cha Igamba ambao ni wakulima wa Kahawa wakipiga picha ya pamoja baada ya kupata elimu na kujiunga na NSSF kama wanachama wa Hiari chini ya Mpango wa Wakulima Scheme ambao utawasaidia Kupata Matibabu bure na Kujipatia Mikopo ya pembejeo.
Maafisa wa NSSF mkoa wa Mbeya wakiwaandikisha watu kutoka Sekta binafsi waliokusanyika kwenye kituo cha mabasi cha mbalizi kwenye kampeni maalum ya NSSF ya kutoa elimu na kuandikisha wanachama Mkoani mbeya ili kuongeza wigo wa wanachama.
 Meneja wa NSSF Mkoa wa mbeya, Robert Kadege akimsaidia mmoja wa Madereva wa Bodaboda kujaza fomu ya NSSF kwa ajili ya Kumuandikisha kujiunga na NSSF.
 Meneja Kiongozi Masoko na uhusiano wa NSSF Eunice Chiume na Meneja wa Mkoa wa Mbeya Robert Kadege wakitoa elimu kwa dereva wa daladala mkoani Mbeya kwenye kampeni maalumu ijulikanayo kama NSSF Kwanza iliyolenga kuwafikia watu walio kwenye sekta binafsi ili wajiunge na NSSF.
Wananchi: Wananchi wa Mkoa wa Mbeya wakiwa wamekusanyika kwenye banda la NSSF ili kupata elimu na kujiandikisha na Mfuko huo eneo la stendi ya Magari ya Mbalizi Mkoani Mbeya.

No comments:

Post a Comment

Pages