Na Talib Ussi, Zanzibar
Mkurugenzi wa Kampuni
ya UR, Salum Mussa Omar ametoa jumla ya Tsh 15 milioni kwa ajili ya mchango wa
Madawati katika Mkoa wa Mjini Magharibi
Zanzibar ambao unakabiliwa na upungufu wa madawati 35,000.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea
msaada huo Mkuu wa Mkoa huo Ayoub Muhammed mahmoud alisema upungufu huo umepelea wanafunzi wengi Mashuleni kukaa chini
sakafuni.
“tatizo hili ili tuweze kuliondoa basi lazima tupate madawati 35 alfu kwa mjini na maeneo mengine 15 alfu” alielezea Mahmoud.
“tatizo hili ili tuweze kuliondoa basi lazima tupate madawati 35 alfu kwa mjini na maeneo mengine 15 alfu” alielezea Mahmoud.
Alisema wamegundua
kukosekana kwa vikalio katika shule
nyingi mjini hapa unaoneka kuwa chanzo chengine cha kushuka kiwango cha elimu.
Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa huyo alieleza kuwa licha ya upungufu huo wa madawati bado sekta ya Elimu inakabiliwa na changamoto nyengine kubwa ikiwemo uchache wa Majengo.
Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa huyo alieleza kuwa licha ya upungufu huo wa madawati bado sekta ya Elimu inakabiliwa na changamoto nyengine kubwa ikiwemo uchache wa Majengo.
“Kwa mfano huu mkoa
wetuu tuu pekee unaupungufu wa vyumba
vya madarasa 144 hali ambayo imepelea darasa moja kuwa na idadi kubwa ya
wanafunzi”aliesema Mkuu huyo wa Mkoa wa Mjini Magharbi.
alieleza kuwa mkoa wake una shule 103 ambazo ni kidogo sana ukilinganisha nan idadi ya wanafunzi ambao wanasoma katika eneo hilo.
alieleza kuwa mkoa wake una shule 103 ambazo ni kidogo sana ukilinganisha nan idadi ya wanafunzi ambao wanasoma katika eneo hilo.
Mapema Mkurugenzi wa kampuni ya UR alieleza kuwa ametoa mchango huo kutokana kuwa elimu ndio mtaji wa kuendeleza Taifa ndio na kampuni yake ikaona ni vyema kutoa mchango huo.
“kama tunataka taifa imara na elimu bora ni vyema kuwekeza katika elimu ili wanafunzi wasome bila ya ghofu” alisema Salum Mussa Omar ambaye ni mkurugenzi wa UR kampani.
Kama ilivyo kwa Tanzania
bara na Rais wa Zanzibar Ali Muhammed
Shein alitoa ombi la raia wema kujitokeza kuchangia madwati kutokana upungu
uliopo.
No comments:
Post a Comment