HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 26, 2016

MTUHUMIWA KESI YA MWANGOSI HUKUMU JULAI 27

Baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi mkoa wa Iringa wakilisindikiza gari lililombeba mtuhumiwa kwa lengo la kuzuia wanahabari wasipate picha.
Baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi mkoa wa Iringa wakiwa wamemzingira mtuhumiwa wa kesi ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Chanel 10 mkoani Iringa, Daudi Mwangosi,Pasificus Simon asipigwe picha na waandishi wa habari wakati akirudishwa mahabusu. (Picha na Denis Mlowe)

NA DENIS MLOWE, IRINGA.

 MAHAKAMA Kanda ya Iringa imepanga kutoa hukumu ya kesi ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Chanel 10 mkoani Iringa Daudi Mwangosi, Julai 27 mwaka huu baada ya kumkuta na hatia ya kuua bila ya kukusudia mtuhumiwa Pasificus Simon.

 Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Iringa anayesikiliza kesi hiyo inayomkabili askari polisi, Pasificus Simon, anayetuhumiwa kufanya mauji hayo, Dk. Paulo Kihwelo, aliyasema hayo jana mara baada ya kutoa utetezi wa pande zote na maoni ya wazee wa baraza na kuahirisha kesi hiyo hadi Julai 27 mwaka huu.

Jaji Kihwelo alisema katika kesi hiyo, mtuhumiwa anadaiwa kuwa, Septemba 2, 2012 alimuua Mwangosi bila kukusudia hivyo hukumu ya kesi hiyo itafanyika mahakamani hapo kuanzia saa nne kamili  asubuhi.

Kihwelo alisema kuwa mtuhumiwa aliweza kuepuka ushahidi mwingine uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashitaka lakini upande wa ushahidi aliotoa na kukiri kuua mbele ya mlinzi wa amani umemtia hatiani na mahakama hiyo kumkuta na hatia ya kuua bila kukusudia ambapo hukumu itatolewa siku hiyo.

Alisema mwenye jukumu la kuthibitisha kosa kwa mtuhumiwa ni upande wa mashtaka ambao unatakiwa uthibitishe bila kuacha shaka yoyote kuwa alifanya hivyo na si upande wa mtuhumiwa kuthibitisha kuwa mtuhumiwa hajatenda kosa.

Jaji Kihwelo alitaja vielelezo ambavyo vilipingwa mahakamani hapo na kuifanya mahakama kuwa na mashaka na ushahidi ulioletwa na upande wa Jamhuri kuwa ni ramani ya tukio, taarifa ya uchunguzi ya kifo cha marehemu na kukutwa na hatia katika ushahidi wa ungamo la mtuhumiwa kwa mlinzi wa amani na kitabu cha kuchukilia silaha FFU cha Iringa.

Kwa upande wake wakili wa Jamhuri, Adoph Maganda alisema kwa kuwa mahakama imemkuta hatiani mtuhumiwa ameitaka mahakama hiyo kumfunga kifungo cha maisha mtuhumiwa kwa kupitia kifungu cha 198 cha adhabu za kuua bila kukusudia mtuhumiwa Pasificus Simon.

Akizungumza kwa niaba ya mtuhumiwa, wakili mtetezi wa Pasificus Simon, Lwezaula Kaijage alisema kuwa kwa kuwa mahakama imemkuta na hatia ya kuua bila kukusudia ameiomba mahakama hiyo kutambua kuwa mtuhumiwa bado ni kijana anayetegemewa na ndugu na familia yake na kuiomba kumwachia huru mtuhumiwa.

“ Kwa kuwa mtuhumiwa aliua bila kukusudia na amekwisha tumia miaka 4 mahabusu  naiomba mahakama yako tukufu kumwachia huru mtuhumiwa kwa kuwa bado kijana na familia yake inamtegemea na ana  mtoto mdogo ambaye anahitaji malezi na matunzo kutoka kwa baba” alisema
 Katika hali iliyozoeleka na kama tabia kwa jeshi la polisi mkoa wa Iringa kuwepo ndani na nje ya mahakama zaidi ya raia ya kawaida na kuwazuia wanahabari kufanya kazi zao hali hiyo iliendelea tena siku ya jana kwa wanahabari mbalimbali kunyasisika hadi kutishiwa kupigwa vibao kwa lengo la kuzuia kupiga picha mtuhumiwa.

Aidha hali ndani ya mahakamani hapo ilikuwa ya kushangaza kwa kesi kuendelea kwa mmoja wa askari ambaye ana nyota moja kwenda katika kizimba kuzungumza na mtuhumiwa bila maelezo ya jaji na kumwacha Jaji Kihwelo akimwangalia kwa mshangao askari huyo.

Aidha askari hao walishindwa kuchukua hatua kwa askari wao kupatikana na kosa la kupiga kelele kwa simu zao lakini waliwatoa tu nje tofauti ambapo mwandishi wa gazeti la Habari Leo na mwenyekiti IPC alipozuiliwa kupiga picha kabla mahakama kuanza.

Naye Rais wa shirikisho la vyama vya waandishi wa habari nchini (UTPC) Deo Nsokolo alisema ameshangazwa na jeshi la polisi kuingilia uhuru wa mahakama hadi kufikia hatua ya kutoa maelekezo ndani ya mahakama hiyo kazi ambayo inapaswa kufanywa na afisa wa mahakama na sio jeshi la polisi.

Alisema kuwa kitendo kinachofanywa na jeshi la polisi kuwanyanyasa wanahabari hakikubaliki katika sheria za nchi na kama utpc kitazungumza na uongozi wa jeshi la juu la polisi kuhusu hali hiyo kwani asilimia kubwa ya waliohudhuria kesi hiyo ni askari hivyo kuwaweka katika wakati mgumu wanahabari kufanya kazi yao kwa waledi.

No comments:

Post a Comment

Pages