HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 10, 2017

MWENYEKITI BODI YA USHAURI TEMESA AFANYA ZIARA KARAKANA YA MT DEPOT

 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu kushoto akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa bodi ya Ushauri ya wakala huo Mhandisi Brig. Gen. (Mstaafu) Mabula Berthiraya Mashauri kulia mwenye miwani wakati alipofanya ziara katika karakana ya Mt Depot jijini Dar es Salaam kujionea utendaji kazi wa Karakana hiyo mapema leo.
Meneja wa Karakana ya Mt Depot Mhandisi Julius Humbe (wa pili kulia) akitoa ufafanuzi kwa Mwenyekiti wa bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Brig. Gen. (Mstaafu) Mabula Berthiraya Mashauri (wa tatu kulia) wakati alipokua katika ziara ya kujionea utendaji kazi wa karakana hiyo jijini Dar es Salaam mapema leo. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu.
 Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Sylvester Simfukwe aliyenyoosha mkono akimuonyesha kifaa cha kunyanyulia gari wakati wa matengenezo (car lifter) Mwenyekiti wa bodi ya Ushauri ya wakala huo Mhandisi Brig. Gen. (Mstaafu) Mabula Berthiraya Mashauri (wa pili kulia) wakati wakati alipokua katika ziara ya kujionea utendaji kazi wa karakana hiyo jijini Dar es Salaam mapema leo. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu.
Mafundi wa karakana ya Mt Depot wakiipima vilainishi gari ya serikali iliyopelekwa katika karakana hiyo na kuifunga mara baada ya kumaliza kuifanyia matengenezo ya kawaida. PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA).

No comments:

Post a Comment

Pages