HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 27, 2018

UJERUMANI 'OUT' SENEGAL VITANI

MOSCOW, RUSSIA


WAKATI mabingwa watetezi wa Kombe la Dunia wakiaga mashindano hayo jana kwa kipigo cha mabao 2-o kutoka kwa Korea Kusini, wawakilishi pekee wa Afrika walio na matumaini ya kusonga mbele, Senegal, wanashuka dimbani Juni 28, 2018 kuivaa Colombia.

Mashujaa wa Korea Kusini, ambao walikuwa wanakamilisha ratiba tu jana, walikuwa ni Kim-Young Gwon na Son-Heung Min, ambao walifunga mabao mawili yaliyofanya Ujerumani kufuata nyayo za Ufaransa, Italia na Hispania, watetezi walioshia hatua ya makundi.

Ufaransa ambao walikuwa ni mabingwa  wa fainali za 1998, waliishia hatua ya makundi mwaka 2002, kama ilivyokuwa kwa mabingwa wa mwaka 2006, Italia walioshia hatua ya makundi katika fainali za 2010. Nao Hispania waliotwaa taji 2010, walichemka katika utetezi mwaka 2014.

Tukirudi katika pambano la Senegal, maarufu kama Simba wa Teranga, ndio nchi pekee ya Afrika inayoweza kufuzu hatua ijayo ya fainali hizo, baada ya wawakilishi wengine Misri, Morocco, Nigeria na Tunisia kuyaaga mashindano hayo baada ya kuvurunda katika mechi zao kweye makundi.

Simba wa Teranga, wanaonolewa na nyota wa zamani timu hiyo, Alliou Cisse, wanashuka dimbani Cosmos Arena mjini Samara, kuwavaa Colombia katika mtifuano wa Kundi H, ambako inasaka sare tu dhidi ya miamba hiyo ili kufikisha alama tano na kufuzu 16 Bora.

Wakali hao wanashuka dimbani kuivaa Colombia wakiwa na pointi nne, ilizopata kwa ushindi wao wa mabao 2-1 dhidi ya Poland na sare ya 2-2 walipoumana na Japan, ambako leo wanapambania sare ili kutinga hatua ijayo ya fainali hizo.

Colombia wana pointi tatu walizopata katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Poland, hivyo watakuwa wakipambana kuichapa Senegal, ili kutinga mtoano wa 16 Bora ya fainali hizo za 21 zinazoendelea katika viwanja mbalimbali nchini Russia.

Wawakilishi wengine wa Afrika, Tunisia, wanamaliza mechi zao za Kundi G leo kwa kushuka dimbani kuumana na Panama, pambano la kukamilisha ratiba baada ya kuziaga fainali hizo na kuzifuata Misri (iliyomaliza mkiani Kundi A), Morocco (mkiani Kundi B), Nigeria (nafasi ya tatu Kundi D) na Tunisia (mkiani Kundi H).
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ujerumani, Mesut Ozil, akiwa ameduwaa baada ya kuchapwa na Korea Kusini mabao 2-0.
 Mshambuliaji wa tim u ya taifa ya Korea Kusini, Kim Young-gwon, akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la kwanza dhidi ya Ujerumani katika mchezo wa Fainali ya Kombe la Dunia la Fifa.
Sami Khedira, akiwa amejifunika uso baada ya kupata kichapo kutoka kwa timu ya Korea Kusini.
Mwamuzi wa mechi ya Ujerumani na Korea Kusini, Mark Geiger, akiwataka wachezaji wa Korea Kusini waliokuwa wanashangilia kurudi uwanjani.

 Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Korea ya Kusini, Son Heung, akiwaangalia mashabiki huku akibubujikwa na machozi ya furaha baada ya kuifungia timu yake bao la pili dhidi ya Ujerumani katika mchezo wa Fainali ya Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment

Pages