HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 28, 2018

DTB, Suma JKT Auction Mart ‘zafunga ndoa’

NA SALUM MKANDEMBA

BENKI ya Diamond Trust (DTB) na Kampuni ya Udalali ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (Suma JKT Auction Mart), zimeingia mkataba wa ushirikiano wa kikazi, unaoipa Suma JKT Auction Mart mamlaka ya kukusanya madeni ya benki hiyo.

Hafla ya utilianaji saini ya makubaliano ya ushinrikiano huo yalifanyika jana jijini Dar es Salaam, ambako Mkurugenzi Mtendaji wa Suma JKT Auction Mart, Kapteni Farjara Mkojera, aliahidi utendaji kazi makini, uliojaa weledi, nidhamu na uadilifu.

Kapteni Mjera alibainisha ya kwamba, Suma JKT Auction Mart imejipanga katika kuzisaidia taasisi za kifedha kama DTB, kufanikisha ukusanyaji wa madeni sugu kutoka wa wateja wao, ili kuibakisha na nguvu ya kukabiliana na mchakato wa Tanzania ya Viwanda.

“Kuelekea Tanzania ya Uchumi wa Kati, taasisi za kifedha zimekuwa wahanga wa kutorejeshwa kwa mikopo na kuzikosesha nguvu ya kibiashara, kwa kuzingatia hilo, tukaja na Suma JKT Auction Mart, ambayo imekuja kuziba mianya iliyoachwa na taasisi za udalali,” alisema. Mkojera.

Alifafanua kwamba, Kampuni nyingi za udalali zimekosa weledi, nidhamu, uadilifu na utii katika ukusanyaji madeni, hali inayosababisha wadaiwa wengi kutotendewa haki na kwamba kampuni yake imejikita katika utekelezaji wa majukumu yak echini ya misingi hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Fedha DTB, Joseph Mabusi, alisema makubaliano yao hayo (ambayo hayakuelezwa yatakuwa ya muda gani), hayana maana kuwa benki yake ina madeni mengi yasiyolipika, bali imevutiwa na dira ya Suma JKT Auction Mart.

“Ni makubaliano yanayoifanya Suma JKT kuwa sehemu ya DTB, ikihusika moja kwa moja na ukusanyaji madeni, ingawa hayana maana kwamba tuna wadaiwa sugu wengi. Taarifa za kifedha mwaka uliopita, ziliitaja DTB kama moja ya taasisi chache zenye madeni machache yasiyolipika,” alisema Mabusi.

No comments:

Post a Comment

Pages