HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

October 21, 2018

Pandeni Mti kwa afya zetu: Waziri wa Elimu Zanzibar

Jamii  imeshauriwa kuwa na utaratibu wa kupanda miti kwenye maeneo yao ili  kuhifadhi na kutunza mazingira   kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi yanavyoathiri makaazi ya watu kwa kasi.
Ushauri huo ulitolewa na Waziri wa Elimu na mafuzo ya Amali Riziki Pembe Juma huko Kitope wilaya kasakazini B Unguja wakati akizindua mpango maalumu wa Chuo cha teknologia ya biashara (Microtech) wa kupanda miti zaidi ya alfu 20 katika shule zote za Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Alieleza hivi sasa maeneo mengi watu wameyahama kutokana makaazi yao kuvamiwa na maji ya bahari na kudai kuwa yote hayo yamesababishwa na ukataji miti ovyo ikiwemo mikoko ambayo ipo kwa ajili ya kuzuia mawimbi ya bahari.
“Tupandeni miti kwa ajili ya kulinda mazingira yetu ambayo yatatuwezesha kupata hewa safi na kuepuka baadhi ya maradhi” alieleza Bi Riziki Pembe.
Alieleza kuwa kupanda miti ni sawa na kutowa sadaka  kwa kile alichokifahamisha kuwa wazee walipanda miti miaka mingi iliyopita na hadi leo watu wanaitumia.
“Leo tunakula matunda aina tofauti hii sadaka yenye kuendelea ambayo ilipandwa na mababu na bibi zetu karne kwa karine basin a sisi tuapandeni tukijua kuwa kesho mbele ya mola wetu tunalofungu na hapa duniani tunalinda afya zetu” alieleza Waziri huyo.kuiga upandaji wa miti hiyo.
Aidha wakati akizindua kampeni hiyo  aliwataka wanafunzi wa Shule ya Kitope kuitunza miti hiyo wasome wakiwa katika mazingira salama.
Mkurugenzi wa chuo hicho ambacho kipo Magomeni Zanzibar  Said Saleh Mohamed,  alisema wameamuwa kufanya kazi hiyo kwa sababu bila ya kuwepo mazingira bola hakuna Afya na kama hakuna afya hapana elimu bora.
“Tunawaambia Jamii yetu ya Tanzania kwa ujumla kuwa sisi hatupo kwa biashara pekee bali ni pomoja na kulinda maisha yaliotuzunguka”alieleza Mkurugenzi huyo.
Pia aliitumia fursa hiyo kufiomba vyuo vyengine kuunga mkono kampeni hiyo ili zanzibar na Tanzania iweze kuwa na mazingira salama.

No comments:

Post a Comment

Pages