NA MWANDISHI WETU
KAMPUNI
inayoongoza kwa maisha ya kidigitali nchini, Tigo, imekata kiu ya muda mrefu ya
watumiaji wa simu janja ‘smart phone’ baada ya kuingia makubaliano na Google
kuwapa wateja uwezo wa kulipia maudhui kutoka mtandao wa Google Play Store kwa
njia ya TigoPesa.
Awali,
watumiaji wa simu hizo walikuwa wakitaka kulipia huduma za kununua muziki,
cinema, apps au kusoma maudhui kwenye mtandao wa Google Play Store, walikuwa
wakilazimishwa kufanya manunuzi kwa kutumia kadi ya benki.
Kwa
mujibu wa Mkuu wa Huduma za Kifedha ya Mtandao wa Tigo, Hussein Sayed, huduma
hiyo inayowezeshwa na Bango, inahudumu kwa wateja milioni 7 wanaotumia huduma
ya TigoPesa kulipia maudhui au ‘application’ yoyote inayopatikana Google Play
Store kwa kutumia akaunti ya Tigo Pesa.
“Wateja
wa Tigo wanaotumia simu janja za Android ama tablet, sasa wanaweza kufanya
manunuzi ya moja kwa moja au malipo kwa njia ya kujisajili kupitia Play Store.
Huduma hii inapatikana kwa njia rahisi na haraka mahali popote pale nchini
kupitia TigoPesa.
“Hii
inawapa wateja wetu uwezo zaidi wa kupakua na kufurahia maudhui ya kimtandao
kutoka Google Play Store, huku wakitumia mtandao wetu wa uhakika na wenye kasi
ya juu zaidi wa 4.5G nchini,” alisema Sayed alisema jijini Dar es Salaam.
Suluhisho
hilo linawawezesha wateja kufurahia huduma za manunuzi ya bidhaa na huduma
walizozoea kwa kuunganisha matumizi ya Google Play na Tigo Pesa. Ili
kukamilisha manunuzi mteja anatakiwa kufuata hatua za kawaida za kufanya
manunuzi kwenye Play Store.
Kwa
upande wake, Mahir Sahin, ambaye ni Mkurugenzi wa Google – Huduma za Android
Barani Afrika, alisema: “Tuna furaha kubwa kuungana na Tigo kuzindua ubunifu
huu utakaowezesha wateja wa Tigo Pesa kufanya malipo ya moja kwa moja kwenye
Googe Play Store.
“Hii
itawezesha mamilioni ya Watanzania ambao hawana kadi za benki kufurahia huduma
kamili za maudhui yanayopatikana kwenye Google Play,” alisdema Sahin.
Idadi
kubwa ya Watanzania wanapenda kutumia simu zao za mkononi kufanya manunuzi ya
huduma ya bidhaa, na sasa Tigo inawawezesha kununua maudhui wanayopenda zaidi
kupitia huduma inayoongoza duniani ya Tigo Pesa.




No comments:
Post a Comment