HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 18, 2019

WATUMISHI JIJI LA MBEYA WAWAKUMBUKA YATIMA

NA KENNETH NGELESI, MBEYA
MEYA wa Jiji la Mbeya Devid Mwashilinsdi ameongoza watumishi wa halmashauri ya jiji la Mbeya kutembea kituo cha watoto yatima cha Malezi ya huruma Simike jijini Mbeya na kutoa msaada wa maitaji vyakula,vinywaji na vifaa vya shule.
Akizungumza wakati akikabidhi msaada mwishoni mwa wiki kwa mama mleza wa kituo hicho wa Anna Kasile, Meya Mwashilindi alisema kuwa msaada huo umetolewa na watumishi wa Halmashauri hiyo baada ya kuchangishana fedha na baaye wamenunua mahitaji kwa ajili ya watoto wanao lelewa katika kituyo hicho.
‘Nitumie fursa kuwashukuru watumishi wa Halmashauri ya jiji kwa kuamu kuchangishana pesa na  kununua mahitaji kwa ajili ya watoto wetu wanao lelewa katika kituo hiki’ alisema Mwashilindi.
Mwasdhilinmdi alibanisha baadhi ya vitu vilivyo tolewa na watumishi hao kuwa ni Daftari, Msafuta ta kupikia,Sabuni ya Unga,Sabuni za mche, Mchele,Kuku,na Sukari na soda na pesa taslimu elfu sh.40000/ kwa ajili ya kununulia maitaji mengine.
‘Pesa hizi zimetoka mifukoni mwa hawa watumishi hivyo japo ni kidogo tunaomba upokee na tunaamini vitaweza kuwa saidia vijana wetu’ aliongeza Mwashilindi
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mama Mlezi wa kituo hicho aliwashukuru watumisahi kwa kujaliwa moyo moyo wa huruma na upendo na hatimaye wameweza kuwakumbuka watoto wanao ishi katika mazingira magumu na hatarishi.
‘Nawashukuru sana kwa msaada huu kwani inaonyesha ni jinsi mlivyo na moyo wa huruma na upendo kwa watoto na niwasii muendelee moyo huo huo wa watu wenye mahitaji maana hata maandiko yanatukumbusha atoaye kwa ukarimu hupokea kwa ukarimu msiishie katika kityuo huiki bali hata vituo vingine’ alisema Kasile

No comments:

Post a Comment

Pages