HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 25, 2019

RC MWANRI AAGIZA KUWA NA DAFTARI ZA WAKAZI ILI KUZUIA UHALIFU

 Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, akiwahutubia wakazi wa Kata ya Tambukareli katika Manispaa ya Tabora jana wakati wa kampeni ya kufichua wahalifu katka maeneo mbalimbali mkoani humo.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri (mwenye Tshirt nyeupe), akibadilishana mawazo na wakazi wa Kata ya Tambukareli katika Manispaa ya Tabora jana wakati wa kampeni ya kufichua wahalifu katka maeneo mbalimbali mkoani humo. (Picha na Tiganya Vincent).


NA TIGANYA VINCENT

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora amewataka Wenyeveti wa mitaa na vitongoji kuwa na Daftari la Wakazi wa maeneo yao ili kuwa na orodha ya wakazi wote kwa ajili ya kudhibiti wageni wasio waaminifu kujificha kwenye mitaa yao.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora  Aggrey Mwanri wakati wa kampeni yake ya fukua fukua inayolenga kufichua watu ambao wanaendesha vitendo vya uhalifu kama vile ujambazi, wizi na matumizi ya dawa za kulevya.

Alisema kuwa hatua hiyo itadumisha ulinzi na usalama katika maeneo mbalimbali mkoani Tabora na kuepusha wahalifu kutoka maeneo mengine kukimbilia mkoani humo.

Mwanri aliwaonya wakazi wa Mkoa wa Tabora kutopokea wageni bila kutoa taarifa zinazowahusu kwa viongozi wa mitaa au vitongoji vyao ili kupokea vitendo vya kuhifadhi wahalifu.

“Endapo tutakugundua mkazi kuishi na mgeni bila kutoa taarifa kwa viongozi wa Mtaa tutamchukulia kama mhalifu…ni vema ukipata mgeni useme nina mgeni ameingia leo na anatarajia kukaa katika eneo hilo kwa kipindi gani na ametokea wapi? alisema.

Mwanri alisema uhalifu unaotoea umesababishwa na baadhi ya wenyeji kuwapokea wageni wasio waaminifu na kuwaficha katika nyumba zao hata bila viongozi mtaani kwake kutojua.
Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tabora amepiga marufuku uchezaji wa michezo kama vile bao, karata, na unywaji wa pombe  za asubuhi na muda usioruhusiwa.

Alisema michezo yote itaanza kuchenzwa mchana ili kutoa fursa kwa wananchi kushiriki kazi za uzalishaji mali na kufanyakazi za kujiingizia kipato.

Mwanri alisema kwa upande wa vilabu vya pombe vitaruhusiwa kuuza pombe kuanzia saa 9.30 hadi saa 4.30 usiku kwa siku za kawaida na wikendi na sikukuu watauza hadi saa 6.00 usiku.

Alisema lengo la zuio hilo ni kuepusha baadhi ya watu kutumia maeneo hayo kama sehemu ya kupanga uhalifu na kugeuza maficho ya wahalifu.

No comments:

Post a Comment

Pages