HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 20, 2019

VBC YATOA BAISKELI 100 KWA WANAFUNZI WA KIKE-MULEBA

 Mkurugenzi  wa Shirika la kwa Wazee Nshamba, Bi Lydia Lugazia.
Solar 240 kwa ajili ya watoto kujisomea.

 Mgeni rasmi chrizant Kamugisha.

Meneja wa Mradi wa Vijana Bicycle Center, Adelphinus Alexander.
 
Na Lydia Lugakila 
Ili kukomesha  vitendo vishawishi  vinavyowakumba watoto wa kike wawapo njiani vitokanavyo na  kutembea umbali mrefu kufuata Elimu, shirika lisilo la kiserikali la kwa wazee Nshamba wilayani Muleba mkoani Kagera limetoa baiskeli  100 bure  zenye thamani ya shilingi milioni 15 kwa  wanafunzi wa kike wapatao 100 kutoka shule za sekondari 25 wilayani  humo ili kuwawezaesha wanafunzi hao  kupata elimu bila vikwazo.
Zoezi hilo la ugawaji wa baiskeli bure kwa wanafunzi hao kutoka  shule 25 za sekondari za wilaya hiyo limefanyika Septemba 20, 2019 katika  uwanja wa Zimbihile uliopo wilayani  Muleba kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi hasa wale wanaotembea umbali mrefu kwenda shule na kupunguza mimba za utotoni zinazotokana na vishawishi wavipatavyo njiani.
Adelphinus Alexander ni Meneja wa Mradi wa Vijana Bicycle Centa Center (VBC) chini ya Shirika la kwa Wazee Nshamba amesema kuwa wilaya ya muleba imekuwa ikitajwa mara kwa mara kuhusika na vitendo vya mimba za utotoni jambo ambalo husababisha watoto wa kike kushindwa kufia ndoto zao huku wengi  wakiishia katika vishawishi vya kupewa lifti na waendesha pikipiki ambao huaribu maisha yao kabla ya kutimiza ndoto zao.
Kufuatia hali hiyo Alexander na timu yake kutoka shirika hilo wameamua kupambana vikali ili kutokomeza kabisa vitendo hivyo kwa kutoa Baiskeli 100 kwa watoto hao wa kike toka shule za sekondari 25 za wilaya hiyo ambapo pia zimetolewa taa za solar 240,  mashine 26 za kuongeza usikivu kwa watooto wenye ulemavu pamoja bima za afya zipatazo 60 kwa wanafunzi  kwa ajili ya kujisomea  vitu vinavyokamilisha jumla ya shilingi milioni 23.
Bi Lydia Lugazia ni Mkurugenzi  wa Shirika la kwa Wazee Nshamba amesema shirika hilo limekuwa ni mdau wa maendeleo wilayani hapo kwa kipindi cha miaka 16 ambapo licha ya kujizatiti katika huduma za kuongeza kinga kwa jamii, ikiwemo  kutetea , kulinda na Kusaidia wazee na watoto  lengo lao ni kuongeza ustawi  kisaikolojia katika kuhakikisha watoto wote wananufaika  katika Nyanja ya Elimu.

Bi Lugazia amesema kuwa shilika hilo limekuwa likitoa vifaa vy shule kwa watoto wenye mahitaji maalum ambapo jumla ya walengwa 107 wakiwa wasichana 56 wavulana 51 wanahudumiwa ndani ya Kata ya 6 ambazo ni Ngenge, Biirabo, Mubunda, Kashasha, Nyakatanga na Mshabago

Kwa upande wake  Mgeni rasmi katika zoezi hilo Chrizant Kamugisha ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba amelishukuru shirika hilo katika mapamabano hayo yanayolenga kutokomeza mimba za utotoni na kuyataka mashirika mengine kuiga mfano kama huo na huku akiwahimiza  wazazi wa wanafunzi hao kutotumia baiskeli hizo katika shughuli zao binafsi bali zitumike kwa wanfunzi hao  tu kwenda shule ili kutimiza ndoto zao.

Hata hivyo wadau wa elimu na wazazi wa wanafunzi hao wamewahimiza watoto hao kusoma kwa bidii na kuwa na neno hapana Mdomoni mwao mara wanapokutana na vishawishi vya aina mbali mbali.

No comments:

Post a Comment

Pages