HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 17, 2019

WAANDISHI WA HABARI KAGERA WAASWA

Mwenyekiti wa Club ya Waandishi wa Habari mkoani Kagera,  Mbeki Mbeki (kushoto), akisalimiana na Katibu Tawala Wilaya ya Misenyi, Abdallah Mayomba.


Lydia Lugakila, Bukoba
Waandishi wa habari mkoani kagera wametakiwa kuendelea kutimiza majukumu yao yenye manufaa katika jamii ikiwemo  kuandika habari kwa kufuata maadili katika kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu, ili kufanikisha uchaguzi huo kuwa huru na wa haki.
Kauli hiyo imetolewa leo Septemba 16, 2019 na Mwenyekiti  wa club ya waandishi mkoani Kagera Mbeki Mbeki  wakati akiongea na baadhi ya waandishi wa habari wilayani misenyi mkoani Kagera waliotaka kujua nafasi ya tasnia ya habari  katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mbeki amesema  ni lazima waandishi wa Habari watambue kuwa wafanya kazi chini ya sheria za nchi hivyo wanatakiwa kuepuka kuandika habari zinazoegemea upande mmoja au habari za uchochezi  ambazo haziwezi kuleta matokeo chanya katika jamii.

Kwa upande wake katibu tawala wilayani Misenyi Bwana Abdallah Mayomba amesema serikali wilayani humo itahakikisha inakuwa bega kwa began a waandishi wa habari ikiwemokutoa ufafanuzi wa mambo yatakayohitaji kuhabarisha wananchi.

No comments:

Post a Comment

Pages