HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 29, 2019

WACHEZAJI LUGALO UGANDA WACHUANA VIKALI TANZANIA LADIES OPEN MOSHI

 Wachezaji  Kutoka kulia Merci Nyanchama wa Kenya  Peace  Kabasweka  wa pili kulia wakibadilishana matokeo na Angel Eaton wa kwanza kushoto na Hawa Wanyenche wa pili kushoto wote wa Lugalo mara baada ya kumaliza mchezo kwa Siku ya pili ya mashindano ya wazi ya Wanawake Tanzania katika Uwanja wa TPC Moshi. (Picha na Luteni Selemani Semunyu).
Wachezaji   Merci Nyanchama wa Kenya na Peace  Kabasweka  kulia na  Angel Eaton na Hawa Wanyenche kushoto  wa Lugalo  wakipongezana mara baada ya kumaliza mchezo kwa Siku ya pili ya mashindano ya wazi ya Wanawake Tanzania katika Uwanja wa TPC Moshi  (Picha na Luteni Selemani Semunyu).


Na Luteni Selemani Semunyu

Mashindano ya golf ya wanawake Tanzania yamefikia siku ya pili huku wachezaji kutoka klabu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo wakichuana vikali na mchezaji kutoka Uganda Peace Kabasweka.

Mchezaji huyo wa  Uganda aliongoza tangu siku ya kwanza kwa fimbo mbili dhidi ya Angel Eaton wa Lugalo akifuatiwa na Hawa Wanchenche wa Lugalo pia.

Licha ya kuongoza kwa fimbo mbioli siku ya kwanza mchezaji huyo kutoka uganda alisema bado mchezo ni mgumu na matumaini ya kuibuka na ushindi bado ni magumu na mwamuzi ni siku ya mwisho ya mchezo

“ Wachezaji kutoka Lugalo ni Wakali na Wanajituma  na Idadi ya Fimbo ninazoongoza ni chache hivyo ukifanya mzaha kidogo basi ni rahisi kufungwa hivyo bado naweza kusema Mchezo ni Mgumu” Alisema  Kabasweka

Naye Mchezaji kutoka Lugalo Angel Eaton  aliyekuwa akimfuatia alisema peace ni Mchezaji mzuri na mchezo bado uko upande wake lakini hakuna kukata tamaa mpaka dakika ya mwisho.

“ Nimetumwa na klabu yangu ushindi hivyo nitapambana kuhakikisha  ubingwa unakwenda lugalo mengine tumwachie mungu kwani kuna wachezaji wazuri tu na wanacheza vizuri mpaka sasa “ Alisema Angel.

Kwa Upande wake mchezaji Hawa Wanchenche naye kutoka  kutoka klabu ya Lugalo  alisema wamepangwa kundi moja leo kutokana  na mchezao mzuri na hapa tunawania ubingwa lakini pia nafasi kushiriki mashindano nchini Uganda.

Kutoka Kenya ambao nao wameshiriki  katika mashindano haya mchezaji Merci  Nyanchama kutoka kwa upande wake alisema amecheza vibaya hivyo hana matumaini ya ushindi lakini kiujumla mashindano ni mazuri na yamevutia.

No comments:

Post a Comment

Pages