HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 02, 2019

SHULE ZA MSINGI 981 KAGERA KUPEWA VYANDARUA

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Marco Mbata (aliyesimama), akitoa maelezo kuhusu uzinduzi wa vyandarua katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kagera.


Na Alodia Dominick, Bukoba

Vyandarua vyenye viuatirifu vya kuuwa mbu waenezao maralia vipatavyo 348,380 vimeanza kugawiwa  katika shule zote za msingi zipatazo 981 katika Mkoa wa Kagera.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Marco Mbata, akitoa taarifa kwa mkuu wa mkoa huo amesema kuwa, zoezi la kugawa chandarua  limeanza  septemba 30 Mwaka huu na litaisha Octoba 10 mwaka huu.

Mganga Mbata ameongeza kwamba, wanafunzi wametumika kama njia ya kufikisha chandarua kwenye familia na kuwa wanafamilia wanapaswa kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo.

Na kwamba ugawaji huo kitaifa ni awamu ya saba na katika mkoa wa Kagera ni awamu ya tatu.

Kwa upande wa mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti ameeleza kuwa, jitihada za serikali ni kuhakikisha ugonjwa huo unatokomezwa na kuwa mwaka 2015/2016 maambukizi yalikuwa ni 41% na mwaka 2017/2018 maambukizi ya maralia yalikuwa 15.4%.

Aidha Brigedia Gaguti amesema dhamira ya serikali ni kufikia mwaka 2020 maambikizi ya Maralia yawe chini ya asilimia 1 na malengo ya kitaifa kufikia mwaka 2030 ugonjwa wa maralia uwe umetokomezwa kabisa.

Hata hivyo mradi huo unatekelezwa na serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa ufadhiri wa serikali ya Marekani kupitia shirika la misaada la watu wa marekani USAID.

Kauli mbiu " Zero Maralia inaanza na mimi".

No comments:

Post a Comment

Pages